![]() |
Wakazi
wa Jimbo la Twaraj Indonesia, wamejiweka utamaduni wa kuwafufua
maiti(wafu) na kuwapamba kwa kuwavisha mavazi mapya, kuwachana nywele na
kuwatembeza mitaani kabla ya kuwazika tena
|
|
Dunia
imejaa vituko na matukio ya ajabu, hilo limedhihirika hivi karibuni
huko nchini Indonesia, katika jimbo la Twaraj, wakazi wa eneo hilo
wanatamaduni ya ajabu na ngeni duniani, wakazi hao wanawafufuwa maiti
kaburini na kuwavalisha nguo mapya za thamani, kuwachana nywele na
kuwapamba kamalive walivyokua hai. Wakazi hao wanakusanyika na kumfanyia sherehe kubwa maiti kabla ya kuanza msafara wa kumtebeza katika mitaa na kumrejesha kaburini alipokuwa amezikwa, wakazi hao wanamini kwamba watu waliyokufa wanahaki ya kuendelea kuishi na kujumuika nao. katika kufanikisha zoezi hilo la kihistoria ambalo wanaimani kwa lazima kufanya ili kuonesha hishima kwa maiti na kulinda mapenzi ya kweli kwa mtu aliyekufa, kabla ya kumzika maiti anavishwa kitambaa maalum ili kuzuia mwili wa marehemu kuoza. |

Timu ya soka ya Zanzibar
Shirikisho la mchezo wa Soka
visiwani Zanzibar,ZFA limechukua uamuzi ambao umewashngaza sana
mashabiki wengi wa soka, visiwani humo, nchini Tanzania na barani Afrika
kwa ujumla.
Kwa mujibu wa ripoti maafisa wakuu wa ZFA
wamewapiga marufuku wachezaji wake wote walioshiriki katika michuano ya
kuwania kombe CECAFA Senior Challenge, iliyokamilika nchini Uganda,
kutoshiriki katika mechi yoyote popote duniani kwa muda usiojulikana.Aidha ZFA limeamua kuvunja timu ya taifa maarufu kama Zanzibar Heroes, licha ya kuwa timu hiyo ilimaliza katika nafasi ya tatu katika michuano hiyo ya CECAFA.
Baadhi ya wachezaji hao waliopigwa marufuku ni pamoja na nyota na naodha wa Yanga, Nadir Haroub.
Kwa nini ZFA ilichukua hatua hiyo?

Nadir Haroub naodha wa Yanga
Akitoa tangazo hilo, katika makao makuu ya shirikisho hilo, makamu wa rais wa ZFA Alhaj Haji Ameir, alisema wanachama wote wa kamati kuu ya ZFA kwa kauli moja waliafikiana kuhusu hatua hiyo, ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine.
Kamati hiyo ya ZFA iliitisha kikao cha dharura, baada ya wachezaji hao wa Zanzibar Heroes, kugawana fedha walizoshinda wakati wa michuano hiyo ya CECAFA.
Zanzibar ilimaliza katika nafasi ya tatu na hivyo kujishinda dola elfu Kumi za Kimarekani.
Ripoti zinasema fedha hizo ziligawanywa na wachezaji hao kama njia moja ya kuwasilisha malalamishi yao kwa ZFA kuhusiana na jinsi wao wanavyoshughulikiwa wakiwa kambini.
Inadaiwa kuwa wachezaji hao waliamua kugawana fedha hizo kwa madai kuwa wamekuwa wakidhulumiwa fedha zao na ZFA.
Baadhi yao wanasema ZFA huwa na mazoea ya kuchukua hela zote wanazoshinda bila hata kuwapa chochote ili hali wao ndio waliofanya kazi zaidi.
Kinyume na matarajio ya wengi kocha mkuu wa Zanzibar Heroes, Salum Bausi ambaye kujiuzulu baada ya mashindano hayo ya CECAFA, amewashangaza wengi kwa kuunga mkono, uamuzi huo akisema wachezaji hao wameharibu sifa ya Zanzibar.
Hata hivyo kuna baadhi ya wachezaji walioamua kurejesha fedha walizopewa kwa shirikisho hilo na ZFA haijatoa orodha yao.
CHANZO:BBC