Wednesday, December 12, 2012

Waliopata kikombe cha Babu wazidi kupoteza maisha

Kwa ufupi
Masinde alisema idadi ya vifo vilivyotokana na Ukimwi katika wilaya hiyo katika kipindi hicho, vimeongezeka kwa asilimia mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.
 IDADI ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ukimwi katika Wilaya na Mkoa wa Geita, inasemekana imeongezeka katika kipindi cha mwaka 2011/12 kufuatia hatua ya baadhi ya wagonjwa, kuacha kutumia dawa za kupunguza makali ya virusi baada ya kwenda Loliondo kwa babu na kupata kikombe cha dawa.
Hali kadhalika kuwapo kwa shughuli za migodi ya wachimbaji wadogo na uvuvi katika Ziwa Victoria, kumechangia ongezeko la vifo vya watu kutokana na ugonjwa huo.
Imeelezwa kuwa ongezeko la shughuli za kiuchumi katika maeneo ya madini na uvuvi, ni changamoto kubwa kwa idara ya afya wilayani humo  katika kupambana na kasi ya maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa Ukimwi kwa wakazi wa Geita.
Mratibu wa Mpango wa Kudhibiti Ukimwi katika Wilaya ya Geita, Patrisia Masinde, aliiambia Mwananchi jana kuwa katika kipindi cha kati ya  Januari na Novemba mwaka huu, watu 31 walipoteza maisha kutokana na ugonjwa huo ambao hadi sasa haujapata tiba. Alisema watu hao ni  sehemu ya watu 131,waliokuwa wamelazwa katika vituo vya afya wakipata huduma.
Masinde alisema idadi ya vifo vilivyotokana na Ukimwi katika wilaya hiyo katika kipindi hicho, vimeongezeka kwa asilimia mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana.
Kwa mujibu wa mratibu huyo, katika kipindi hicho mwaka jana, watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa huo walikuwa 16.
Kwa upande wake, Mratibu wa Ukimwi katika Kitengo cha Matibabu katika Wilaya ya Geita, Dk.John Mgosha alisema vifo hivyo vinatokana na baadhi ya wagonjwa waliokwenda kwa Babu wa Loliondo na kupata kikombe cha dawa, kuacha kutumia vidonge vya kuvumbaza virusi vya Ukimwi.
Alisema baadhi ya watu hao  Loliondo waliamini kwamba Mchungaji Amilikile Masapila, alikuwa na dawa ya kutibu ugonjwa wa Ukimwi licha ya kutambua kuwa hakuna dawa iliyothibitishwa na watalaamu wa afya kutibu ugonjwa huo.

MNYIKA AWATAJA MAFISADI TANESCO

Kwa ufupi
Mnyika aliwataja vigogo wengine watatu wa Tanesco na kueleza kuwa walifanya uzembe na kushindwa kusimamia sheria ya ununuzi wa umma na kupendekeza kampuni mbili kupewa zabuni, licha ya kuwa hazikutimiza masharti kwa sababu ya mgongano wa maslahi
 MBUNGE wa Ubungo John Mnyika

MBUNGE wa Ubungo John Mnyika, ametaja majina ya watu 16 ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambao amewahusisha na ufisadi ndani ya shirila hilo la umma.
Mnyika ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Madini na Nishati alisema watu hao ndio wanaoshirikiana kuihujumu Tanesco na kuliingiza taifa katika hasara.

Kati ya majina hayo ambayo ameyaita kuwa ni ya awamu ya kwanza wamo baadhi ya waliokuwa watendaji wa shirika hilo ambao wamesimamishwa kupisha uchunguzi unaofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).

Alipoulizwa wiki iliyopita kuhusu uchunguzi huo, GAG Ludovick Utouh alisema uchunguzi huo umeshakamilika na kilichokuwa kikisubiriwa ni kuikabidhi ripoti hiyo kwa bodi ya Tanesco.

Mnyika aliwataja vigogo wengine watatu wa Tanesco na kueleza kuwa walifanya uzembe na kushindwa kusimamia sheria ya ununuzi wa umma na kupendekeza kampuni mbili kupewa zabuni, licha ya kuwa hazikutimiza masharti kwa sababu ya mgongano wa maslahi.

Mnyika alipendekeza vigogo hao kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Aliwataja watumishi wawili ambao walishindwa kutoa taarifa za ukiukaji wa vigezo vya utoaji wa zabuni namba PA/001/09/HQ/W/014 na kufanya kampuni moja kati ya hizo mblii kupewa zabuni.

Alisema watendaji hao walichangia kufanya kampuni hiyo kupewa zabuni pamoja na kwamba haikuwa na fedha na kuiwezesha kupewa malipo ya asilimia za ziada kinyume na mkataba.

Akapendekeza watendaji hao kuchuliliwa hatua za kinishamu. nMnyika aliwataja watumishi wengine sita wa Tanesco ambao kwa pamoja walifanya uamuzi uliosababisha kutolewa kwa mkataba namba PA/001/HQ/W/14 wa Machi 11,2010 kwa kampuni hiyo bila kuzingatia uwezo wa kitaalam, kifedha na hivyo kukiuka sheria ya ununuzi wa umma.

Alisema hao wanatakiwa kuchukuliwa hatua ili kuwadhibiti watumishi wa umma wanaoliingiza taifa katika mikataba mibovu.

Mnyika katika taarifa yake hiyo aliwataja wafanyakazi watatu wa Tanesco akieleza kuwa walihusika katika kutoa mapendekezo yaliyowezesha kampuni ya McDonald kupewa mkataba wa zabuni kinyemela.

Mnyika alipendekeza wachukuliwe hatua za kisheria ili kuepusha Tanesco kuingia mikataba kuliongezea shirika mzigo wa gharama na kusababisha ongezeko la bei ya umeme.

Mkutano wa katiba Z’bar vurugu tupu


Kwa ufupi
Baadhi ya maeneo ambayo wanasiasa hao walivamia mikutano ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kusababisha ivunjike ni Shehia za Magomeni na Mpendae Mkoa wa Mjini Magharibi.Hii ni mara ya kwanza ghasia kuzuka katika mikutano ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya visiwani humo.
MIKUTANO ya kukusanya maoni ya upatikanaji wa Katiba Mpya Visiwani Zanzibar, imeingia dosari baada kuzuka ghasia na baadhi ya watu kujeruhiwa kwa kuchomwa visu.
 Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji warioba 

Vurugu hizo ambazo chanzo chake ni siasa, zilitokana na wafuasi wa baadhi ya vyama vya siasa, kuvamia mikutano iliyokuwa ikifanyika Unguja na kusababisha hofu za kiusalama.

Baadhi ya maeneo ambayo wanasiasa hao walivamia mikutano ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kusababisha ivunjike ni Shehia za Magomeni na Mpendae Mkoa wa Mjini Magharibi.Hii ni mara ya kwanza ghasia kuzuka katika mikutano ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya visiwani humo.

Tukio la kuchomana visu, lilitokea katika Shehia ya Mpendae baada ya vurugu zilizosababishwa na vijana kuvamia mkutano uliokuwa ufanyike jana mchana.
Vijana hao walianzisha ghasia hizo baada ya kutaka kuvunja utaratibu uliokuwa umewekwa. Walitaka wakae mbele ya wengine waliokuwa wametangulia katika mkutano huo.

Hatua hiyo ilipingwa na kuibua ghasia ziliozababisha watu kadhaa kujeruhiwa kwa visu.

Tukio jingine lililovuruga mkutano huo ni lile lililotokea katika Shehia ya Magomeni, Jumatatu wiki hii baada ya kuibuka kwa mvutano baina ya makundi mawili yenye misimamo tofauti juu ya mfumo wa Muungano; kuna wanaopinga na wanaoukubali.
Misimamo hiyo imeelezwa kujikita katika misingi na sera za vyama vyao vya kisiasa.
Katika misimamo hiyo, CUF kinaamini katika Serikali ya Zanzibar na Tanganyika kila moja kuwa na mamlaka kamili na Muungano uwe wa mkataba wakati, CCM kinasimamia kwenye Serikali mbili; Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Shehia ya Magomeni
Saa mbili kabla mkutano kuanza, watu wengi walifika Uwanja wa Mzalendo ambako mkutano ulitakiwa kufanyika. Walijipanga kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na Tume ambao ni aliyewahi kufika ndiye anayetangulia kutoa maoni.

Hali hiyo ilisababisha wakazi wa Shehia hiyo waliokuwa wenyeji wa mkutano, kukosa nafasi ambayo ingewawezesha kutoa maoni kwa mazungumzo ya ana kwa ana.
Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni, Salmin Awadh Salmin, alisema hawakuwa tayari kuwa wenyeji wa mkutano ambao hawatashiriki akisema waliokuwa wamejipanga wote walifikishwa kituoni hapo kwa magari kwa lengo maalumu la kuwakosesha wenyeji kutoa maoni yao, kwa kuwa inafahamika kuwa wengi wao ni wana CCM.

Hoja hizo alizitoa kwa wajumbe wa Tume ambao pia hawakuridhishwa na hali ya usalama katika eneo hilo kutokana na vurugu zilizokuwa zikifanywa na wafuasi wa CCM na CUF.

“Kwa hali ilivyo, hatuwezi kupata utulivu utakaowezesha tufanye kazi kwa ufanisi na kumaliza mkutano kwa amani bila fujo. Natangaza rasmi kuwa leo hakuna mkutano,” Mwenyekiti wa Timu ya Tume hiyo inayokusanya maoni visiwani hapa, Profesa Mwesiga Baregu.

Akizungumza baada ya kuvunjika kwa mkutano huo, Salmin alisema waliokuwa wamefika kutoa maoni walikuwa wakitaka kunadi misimamo ya vyama vyao akisema hiyo ni hali ya kihistoria inayowakabili wakazi visiwani humo.

WHY GIVE UP?



   
 IF I knew a person who was always giving up then that’s me!
      If I was asked to mention one person that can even take her life because of giving up; I won’t think twice that would still be me.
      One day I asked myself; why should I give up all the time? Why is it that I always feel very discouraged when I do one wrong move?
       I once listened to one person preaching and he said that up there in heaven there are many souls of different people and that when your time to be born comes God calls by name and gives you a mission on Earth to fulfill- I don’t know if it’s true or not but it gave a point of thinking.
        We all have plans; thoughts and goals we want to meet; not only meet but meet them at maximum achievement. But there are times that we achieve zero or not to the level we imagined. You know it’s everybody’s right to dream, dream of anything, with any size; too small; too big they are all dreams. But can we achieve all that we dream about? Some people give up when they fail, they lose hope to try again. This is not very wise because God is the one who plans for our lives even before we plan. He knows who we are and why he created us.
         As long as sun shines at the day; the moon at night; then God is there; there is no reason to give up with God in charge for he knows our future. He won’t leave us just because we failed. He doesn’t count how many times we don’t finish the race well; what matters to him is that we took the race. If you are still alive; there is still an opportunity for you to get a second chance; still an opportunity to fix what was destroyed don’t give up.
         Why give up when you’re not alone? If you give up that means you don’t trust yourself and God who’s always by your side. He is there, he is real; and success is a must.
He never did grant anyone a peaceful and smooth journey; every champion has his own valleys different from any other. Experience shows that when your valley is more deadly the more you get promoted. Just don’t give up.
         The darker it gets the sooner the morning comes; the more the intense the pain the more the success.
Abraham-no children for years
Jacob-his only brother wanted to kill him.
Joseph- his brothers hated him.
Moses-the king wanted him dead
Jesus-killed by the Israelites (his own people)
        Everyone has his challenges; they are never the same to everyone. But what’s common is that God saves us from all those. If he raised Jesus from the dead; can’t he handle your problem!?Is it that big to him??
          Some of us just succeeded by going low first; Jesus went low as dying and got raised as high as the heavens.
         Being low does not mean you lost; it’s only a bent not the end. Struck down but not destroyed; Raise up; Gather strength; face the next level GOD was not wrong to choose you only you can play your role well
        Sometimes God breaks our spirits to savior souls. Sometimes he breaks our hearts to make us whole sometime he allows pain so as to be stronger
Sometimes he sends us failure so that we can be humble.
He sometimes takes away everything from us so as to make us learn the value of everything he gave us.
       Life is the hardest subject than all. In other subjects we learn first then test later but life is a test first; lesson later. We can’t be afraid to make mistakes; they are our only ways to learn how to be perfect.

Don’t fight your weakness; fight to win because God uses your weaknesses to raise you high.
                              Prepared by HEAVEN DAVID