Friday, January 25, 2013

PICHA MBALIMBALI ZA MAANDAMANO YA WANACHUO WA ST.JOHN YALIYOFANYWA KATIKA SIKU YA JANA

Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Wanafunzi baada ya kusubili kwa muda mrefu kibari icho wakaamua kuandaa mabango kwa ajili ya maandamano, ambapo kibari kipatikane kisipatikane walidai kuandamana ni lazima






Mabango yalipokamilika wakasimama kwenye bendera kwa mara nyingine







 
Walifika mbali na kuona kuwa polisi wanahusika katika mambo mabaya wanayofanyiwa. Ndipo wakachora bango hili kuonyesha hisia zao
Hapa wapo barabarani na masomo kwa siku ya leo hayakuwepo


Bango lina picha ya mwanafunzi alieuliwa kikatili, aliefahamika kwa jina la LYDIA LEO




Ni mchaka mchaka ulioendana na nyimbo za hisia



Haya huyu anaashiria demokrasia na maendelea ndio imetawala juu yao

Msafara hapa unaelekea maeneo ya Bungeni

Kila walipopita walikuwa wakishindikizwa na polisi kuhakikisha amani inatawala

Hakuna kitu ambacho kiliniacha hoi baada ya wanafunzi kwenda mpaka Bungeni, kisha walipofika wakaimba nyimbo ya Taifa. Polisi waliwaomba kuongea na viongozi wa maandamano hayo wakajibiwa na wanafunzi kuwa kiongozi wao hameishakufa ambae ni mama LYDIA LEO

Gari la maji ya kuwasha lilikuwepo lakini wanafunzi hao hawakutishika na kitu chochote kile kutoka kwa Polisi


Wanafunzi walifika mpaka Nyerere Square waliimba nyimbo mbalimbali mahala hapo





Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Gari la washa washa nalo lilikuwepo lakini watu walikuwa na jaziba zao vilevile mwanzo mwisho

Barabara zilikuwa zimetawaliwa na wanafunzi kwa kiasi kikubwa, mpaka kusababisha magari kutopita



Hapa ndipo safari ya maandamano ilipoanzia na ndipo safari hiyo ilipoishia maeneo haya ya kwenye bendera mbele ya jengo la administration.

Safari ya maandamano ya amani ikawa imeishia chuoni hapo baada ya kuona kuwa ujumbe wao umefika. Wanafunzi wa chuo wamechoshwa na matendo mabaya ambayo wanafanyiwa ikiwa ni pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kuibiwa vitu vyao kama Laptop na vitu vingine. Wameonesha umoja wao kwa sababu ya kuchoshwa na mambo hayo, ambapo leo asubuhi kuna wanafunzi walivamiwa na kuibiwa Laptop. Hivyo wakaamua kujikusanya asubuhi hiyo hiyo mida ya saa kumi na mbili alfajili na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye walimpiga na baadae kuchukuliwa na polisi.

Thursday, January 24, 2013

WANAFUNZI WA ST JOHN DODOMA ZAIDI YA 5000 WAMENDAMANA KATIKATI YA MJI WA DODOMA WAKIPINGA UBAKAJI NA ULAWITI:

Wanafunzi wa Saint John University wakiwa wamebeba mabango katika maandamano yaliyofanywa leo
Hivi ndivo ilivyokuwa katika mji wa Dodoma kufuatia maandamano  wanafunzi wa Saint John University

Hayo ndiyo yalikuwa ya moyoni mwa wanafunzi wa chuo cha Saint John Dodoma



 
        W anafunzi zaidi ya 5000 wa chuo cha Saint John Dodoma wameandamana leo kushinikiza Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma liwajibike katika matukio ya kiuhalifu yanayoendelea kutokea ndani ya chuo yakiwemo mauaji yanayofanywa na vibaka na majambazi.
         Maandamano hayo yamefanywa kutokana na kudaiwa na wanafunzi hao kuwa kumekuwa hakuna uwajibikaji wa Jeshi la Polisi katika usalama wao.
          Jumatatu ya wiki hii nikimaanisha Tarehe 21 / January / 2013 mwanachuo aliuawa na kuporwa simu,siku ya jana katika Hosteli za akina dada zilivamiwa Laptop , simu na fedha ziliporwa, katika tukio hilo la jana wanfunzi walipigwa na kujeruhiwa vibaya.
           Mkuu wa polisi mkoa wa Dodoma ameahidi kulifanyia kazi tatizo hilo na kuimarisha ulinzi chuoni hapo.

ULINZI WAIMALISHWA KWA WANAFUNZI WA IFM BAADA YA KASHFA YA UBAKAJI NA KUIBIWA NA VIBAKA



UONGOZI wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Usimamazi wa Fedha (IFMSO) cha jijini Dar es Salaam, umesema hali ya usalama kwa sasa katika Hosteli za Kigamboni inaridhisha.
Waziri Mkuu wa IFMSO, Daniel Sarungi alisema jana kuwa tangu iundwe timu ya polisi inayoshirikiana na wanafunzi hao hali imekuwa tulivu kwa kipindi cha wiki moja iliyopita. 
Sarungi alisema kuwa hakujatokea uvamizi tena katika hosteli zao, lakini akaongeza kusema kuwa taarifa kamili ya ripoti ya timu hiyo itatolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova.
“Kuna amani sana, misako imefanyika lakini ripoti itatolewa Januari 30 na Kamanda Kova,” alisema Sarungi.
Kauli ya Kiongozi huyo wa wanafunzi haikutofautina na ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Temeke, Englbert Kiondo, ambaye alisema taarifa inayohusu hali ilivyo itatolewa na Kamanda Kova.

Kwa upande wa wakazi wa Kigamboni, walisema kuwa wameshuhudia polisi wakifanya doria maeneo hayo tofauti na ilivyokuwa huko nyuma kabla wanafunzi hawajaandamana.
Walisema pia wameona polisi wakiwakamata wahalifu kwenye maeneo hayo kutokana na misako wanayoifanya hali ambayo imeleta utulivu kwenye mji huo.
“Kwa sasa kumetulia inawezekana wanasikilizia (wahalifu), likini ingetakiwa polisi wawakamate wale vinara kwa sababu wanawafahamu” alisema Salum Rashid mkazi wa eneo hilo.
Naye mkazi mwingine anayejishughulisha na biashara ya kioski, alisema kuwa kumekuwa na utulivu kwani hata wanafunzi ambao ndiyo wateja wake wakubwa wanamwambia kuwa wanaweza kuacha vitu wakavikuta salama.

Mkasi - SO3E09 with Hasheem Thabeet ( JIFUNZE KWA WALIOFANIKIWA )

NEW VIDEO : SEMINDE FT MUBBYZOW - BATA

WANANCHI WAVAMIA KITUO CHA POLISI NA KUCHOMA NYUMBA ZAO


Habari iliyotufikia hivi punde inaeleza kuwa kundi kubwa la wananchi waliojawa na ghazabu Wilayani Rufiji leo wamevamia kituo cha Polisi Kibiti Wilayani humo na kuanzisha vurugu kubwa kufuatia raia mmoja mkazi wa kijiji hicho kudaiwa kufa kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kipigo cha Polisi.

Chanzo chetu cha Habari kutoka Kibiti kinatupasha kuwa,kijana huyo aliyefariki kutokana na kipigo hicho afahamikae kwa jina la Hamis Mpondi ambaye mauti yamemfika wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili,jijini Dar es Salaam na taarifa hiyo ilipowafikia wananchi hao ndipo wakachukua uamuzi wa kwenda kituoni hapo na kuanzisha vurugu hizo.

Habari zaidi zinaeleza kuwa,hivi sasa wananchi hao wanateketeza nyumba za Askari Polisi hao zilizopo jirani kabisa na kituo hicho, licha ya juhudi za Polisi kuwatawanya kwa mabomu kuendelea kufanyika.

Aidha wananchi hao wameanza kufunga barabara kuu ya Kilwa iendayo Mikoa ya Kusini, Lindi na Mtwara kwa mawe, magogo na kuchoma matairi ikiwa ni umbali wa kama kilometa moja kutoka kituo cha Polisi Kibiti.

Inaelezwa kuwa hali imezidi kuwa tete katika eneo hilo huku Polisi wa Kibiti wakiendelea na jitihada za kudhibiti hali hiyo kwa kufyatua mabomu ya machozi hewani kujaribu kutawanya umati huo wa watu.

tutaendelea kupeana taarifa zaidi kadri zitakavyokuwa zikitufikia.

NEW TRACK : NOORAH aka BABA STYLZ ft ALI KIBA -NIKUPE NINI

KEISHA FT DIAMOND - NIMECHOKA ( OFFICIAL VIDEO )

NEW VIDEO: 50 Cent ft. Snoop & Young Jeezy - Major Distribution

NEW TRACK : NAY WA MITEGO - UTAVUNA ULICHOPANDA

SHINE RECORDS .....TUNA PENDA KUTANGULIZA SHUKRANI ZETU KWA WOTE AMBAO MNATUJALI KWA MAMBO MENGI AMBAYO TUNAFANYA NA PIA TUNAPENDA KUOMBA MSAMAHA KWA WOTE AMBAO TULIWAKERA NA KUTUHISI TUNAWADHARAU NA TUNAPENDA KUTAMBULISHA NGOMA MPYA YA MSANII ..NEY WAMITEGO AMBAYO INA KWENDA NA UJUMBE WA UTAVUNAULICHOPANDA........IKIWA IMEFANYIKA ....SHINE RECORDS.....,,,,CHINI YA MR T....

Tuesday, January 22, 2013

BEN POL FT LINAH - YATAKWISHA ( AUDIO )

Hemedy PHD - Going crazy {Official Video}

SAKATA LA KAHABA ALIYEOKOKA......


Hili ni simulizi la  kweli linalomhusu mwanamke  mmoja ambaye alikuwa ni kahaba  wa makahaba......
Mwanamke  huyu  alijitambua  vyema  na  kukiri  ndani ya  nafsi yake kuwa hawezi  kuolewa  na mwanaume  yoyote  yule  maana  jamii yote ilikuwa inamtambua  kwa uchangudoa  wake......

Kwa hiyo , ili kurahisisha mambo na  kuifanya  biashara  yake  iimarike, mwanadada  huyu aliamua  kwenda hospitali kukitoa  kizazi chake.Hakutaka  tena  usumbufu wa kutoa  mimba  au kufikiria kondomu......

Tangu wakati  ule biashara  yake  iliimarika na wateja  walizidi kumiminika.Baada  ya miaka  kadhaa, Upako  wa  mwenyezi mungu  ulimfikia kupitia kwa mtumishi  mmoja  wa  mungu ambaye  alifanikiwa  kumfanya  aokoke  na  kuwa mtumishi mzuri  kanisani.....
 
Siku moja, mchungaji  mmoja alimwita na  kumwambia  kuwa:
"Dada yangu, Mwenyezi mungu  amenena  na  mimi na  kunifunulia  kuwa  wewe  ndo mke  wangu wa ndoa, hivyo naomba tuoane.."

Mwanamke huyu alitabasamu na kusema:
 "Kaka  yangu, Mungu hajakwambia lolote, lasivyo, utakuwa  hujamsikia vizuri.Naomba  uniache tu maana  sina  mpango wowote wa  kuolewa"

Yule  mchungaji  aliendelea kushikilia  msimamo wake  na  kudai kuwa :

"Mungu  amenifunulia,wewe  ndo  mke wangu" 

Mwanamke  huyu  aliendelea  kuyapuuza  maneno hayo na ndipo sakata  hilo  lilipomfikia  Askofu  wa  kanisa  hilo.....

Wakiwa mbele  ya mchungaji,Mwanamke huyu  alifunguka  kwa  uwazi mbele  ya askofu  na  kudai kuwa kabla ya kuokoka yeye  alikuwa  ni kahaba  wa  makahaba....

Askofu naye alifunguka  na  kudai kuwa :"Sioni sababu ya kuumiza kichwa  kwa  mambo yaliyopita.Mungu  humsamehe  mwanadamu  kwa  kuzifuta  dhambi zake  zote za  nyuma  na  kumfanya  awe  mpya..!!!"

Mwanamke huyu  alifunguka  tena na kudai kuwa:
"Baba  askofu, mimi  nilishatoa kizazi changu  wakati nikiwa  kahaba, kwa hiyo  sitaweza    kuzaa  tena"
Askofu  aliishiwa  pumzi baada  ya kusikia hivyo.Hakuweza tena  kusema  kuhusu  kusahau ya  nyuma.Ilibidi amgeukie yule mchungaji  na  kumwamba: 

"Vipi, bado  kuna maono yoyote  toka  kwa mwenyezi mungu?" 

Mchungaji alijibu  ,"Ndio, huyu ndo mke wangu.."

 Askofu  ilibidi  awaombee kwa  sala  maalumu.Hatimaye ndoa  ikafungwa......Baada  ya  miezi  michachtu, huyu mwanamke  alibeba  mimba.Yeye  pamoja  na mumewe waliongozana pamoja kwenda  hospitalini, tena  kwa  yule  yule doctor  aliyekitoa  kile  kizazi......

Daktari  alipomuona  alifurahi  akidhani kuwa pengine  mteja  wake  kamletea  mteja mwingine.....Doctor  hakuamini  masikio  yake baada  ya kuambiwa kuwa  huyu  mwanamke ni mjamzito na  amekuja  kujiandikisha  clinic....
Hakika Mungu ni  Muweza wa  yote.... 
SOURCE;MPEKUZI