Friday, January 25, 2013

PICHA MBALIMBALI ZA MAANDAMANO YA WANACHUO WA ST.JOHN YALIYOFANYWA KATIKA SIKU YA JANA

Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Wanafunzi baada ya kusubili kwa muda mrefu kibari icho wakaamua kuandaa mabango kwa ajili ya maandamano, ambapo kibari kipatikane kisipatikane walidai kuandamana ni lazima






Mabango yalipokamilika wakasimama kwenye bendera kwa mara nyingine







 
Walifika mbali na kuona kuwa polisi wanahusika katika mambo mabaya wanayofanyiwa. Ndipo wakachora bango hili kuonyesha hisia zao
Hapa wapo barabarani na masomo kwa siku ya leo hayakuwepo


Bango lina picha ya mwanafunzi alieuliwa kikatili, aliefahamika kwa jina la LYDIA LEO




Ni mchaka mchaka ulioendana na nyimbo za hisia



Haya huyu anaashiria demokrasia na maendelea ndio imetawala juu yao

Msafara hapa unaelekea maeneo ya Bungeni

Kila walipopita walikuwa wakishindikizwa na polisi kuhakikisha amani inatawala

Hakuna kitu ambacho kiliniacha hoi baada ya wanafunzi kwenda mpaka Bungeni, kisha walipofika wakaimba nyimbo ya Taifa. Polisi waliwaomba kuongea na viongozi wa maandamano hayo wakajibiwa na wanafunzi kuwa kiongozi wao hameishakufa ambae ni mama LYDIA LEO

Gari la maji ya kuwasha lilikuwepo lakini wanafunzi hao hawakutishika na kitu chochote kile kutoka kwa Polisi


Wanafunzi walifika mpaka Nyerere Square waliimba nyimbo mbalimbali mahala hapo





Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni

Gari la washa washa nalo lilikuwepo lakini watu walikuwa na jaziba zao vilevile mwanzo mwisho

Barabara zilikuwa zimetawaliwa na wanafunzi kwa kiasi kikubwa, mpaka kusababisha magari kutopita



Hapa ndipo safari ya maandamano ilipoanzia na ndipo safari hiyo ilipoishia maeneo haya ya kwenye bendera mbele ya jengo la administration.

Safari ya maandamano ya amani ikawa imeishia chuoni hapo baada ya kuona kuwa ujumbe wao umefika. Wanafunzi wa chuo wamechoshwa na matendo mabaya ambayo wanafanyiwa ikiwa ni pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kuibiwa vitu vyao kama Laptop na vitu vingine. Wameonesha umoja wao kwa sababu ya kuchoshwa na mambo hayo, ambapo leo asubuhi kuna wanafunzi walivamiwa na kuibiwa Laptop. Hivyo wakaamua kujikusanya asubuhi hiyo hiyo mida ya saa kumi na mbili alfajili na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye walimpiga na baadae kuchukuliwa na polisi.

No comments:

Post a Comment