Friday, January 18, 2013

NEW TRACK : JACO BEATS - LOVE IS


                                          SONG : LOVE IS
                                          MSANII : JACO BEATS
                                          PRODUCTION : LONG MILES
                                          PRODUCER : JACO BEATS
   Jaco Beats ni moja ya wasanii wanaofanya vizuri katika industry ya mziki Tanzania. Anafanya vizuri akiwa msanii huku Producer,Mziki wake anaufanya pande za Dodoma.
 

Wednesday, January 16, 2013

New Song: Pnc, Z-Anto, Dogo Janja, Pingu & Cassim - Mtu wa Watu

Artists: PNC, Z-ANTO, DOGO JANJA, PINGU & CASSIM MGANGA
Song: MTU WA WATU

NEW TRACK; SAJNA ft BELLE 9 & PIPI-ROHO MBAYA (PRODUCED BY DUKE)

Baada ya kipindi kirefu kupita msanii Faraji Twaha a.k.a Sajna ameamua kuachia wimbo wake unaoitwa 'ROHO MBAYA' ambao aliurekodi takribani miaka miwili iliyopita na kuwashirikisha Belle 9 pamoja na mwanadada Pipi.
Kwa mujibu wa Sajna wimbo huu sio official single yake ya mwaka huu lakini ameutoa kuvunja ukimya uliotokana na kubanwa na shule na pia kama zawadi kwa fans wake, wakati anajiandaa kutoa official song yake ya mwaka huu 2013. Roho mbaya pia inapatikana katika album yake ya kwanza inayoitwa Iveta.

Tuesday, January 15, 2013

NEW TRACK: MONSTAR - SIJAWASUSA (VUMILIA)

Artist: MONSTAR
Song: SIJAWASUSA (VUMILIA)
Studio: EXPENSIVE MUSIC
Producer: ZIDADAY MWAMBA

HUYU NDIO MWIZI ALIEIBA VITU KWENYE GARI LA MSANII MH TEMBA

Kwa mara ya kwanza juzi january 10 2013 ndio zilitangazwa habari za msanii Mh Temba kuibiwa vitu vya gari lake kwa mara ya tano, amekua na magari tofauti tofauti ambapo kwa mara tano ameibiwa vitu mbalimbali ambapo baadae amekua akilazimika kununua vitu vilevile vya kwake.
Hizi picha amezituma Exclusive kwa millardayo.com na kusema huyu jamaa anatuhumiwa kuwa mwizi hodari wa power window, vioo na vifaa vingine vya magari mbalimbali ambapo alipohojiwa na polisi amesema yeye huwa ananunua tu vifaa vya magari lakini hausiki kufanya wizi.

Wanaofanya wizi ni wengine ndio wanamletea na yeye anafanya kazi ya kumpigia simu mwenye mali ili aje avinunue vifaa vilivyoibiwa kwenye gari lake, sasa kilichofanya Mh Temba amkamate ni pale alipopigiwa simu na huyu huyu jamaa na kudai kwamba anavyo vifaa vilivyoibwa kwenye gari lake.
.

                                                 Hii ndio Verosa ambayo waliiba vifaa ambavyo baadae Temba alikuja kuvinunua kwa laki nane, na ni vifaa vilevile vilivyoibwa kwenye gari lake.
Kumbe huyu jamaa ndio yule yule aliwahi kumpigia simu Temba wakati alipoibiwa tena vifaa vya gari november 2012 na kumuuzia vifaa vilevile kwa shilingi laki nane huku Temba akiitoa hiyo pesa akiwa anajua kabisa vifaa anavyonunua ni vilevile, wakati huu Temba bado alikua ameisave namba yake kwa hiyo akashtukia mchezo kwamba jamaa ndio wanamchezea hivyo akajipanga na kwenda kumkamata.

Mtuhumiwa alipofikishwa polisi akajitetea kwamba yeye hausiki na wizi, yeye anafanya udalali wa kununua na kuuza hivyo vifaa tu na wala vitu vingine vinavyoibwa kwenye magari kama Camera na Laptop huwa hausiki navyo na wala havinunui.
Polisi wanamjua kabisa na namba yake wanayo kwa sababu jamaa amekua na kesi hizo mara nyingi sana hapo kituoni, mara ya mwisho ambapo wengi wanaoibiwa vifaa huwa anawaambia watume pesa kupitia line yake ya simu ya mkononi alafu wakishatuma ndio mtu anatumwa kwenda kuvipeleka hivyo vifaa, kama alivyofanya kwa Mh Temba mara ya mwisho na alitaka kufanya hivyo hata wakati huu.

Mh Temba amerudishiwa vifaa vyake alivyoibiwa wakati huu na mtuhumiwa ameachiwa, sio kwa dhamana ila wamechukua tu alama zake za vidole wakamwambia arudi jumatatu, Temba nae kaambiwa arudi jumatatu.

ALA KICHAPO BAADA YA KUNASWA AKILWAWITI WATOTO WADOGO:


Mwananchi huyu mwenye hasira kali akimnyanyua juu kibaka huyo na kumtupa chini kama akina 'John Cena'.
..Kichapo kikiendelea kwa kibaka huyo.
Kibaka huyo akizidi kuhukumiwa mtaani.
Ustadhi akijaribu kumnusuru kibaka huyo.
Ustadhi huyo aliamua kuondoka na kibaka ili kumwokoa.
Akimpeleka kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na eneo hilo la Shani.
KIJANA mmoja anayesadikiwa kuwa ni kibaka mchana huu amenusurika kifo baada ya kupokea kichapo kikali kutoka kwa wananachi wenye hasira wakimshutumu kuiba watoto wadogo na kwenda nao eneo la mto Morogoro chini ya daraja la Shani na kuwafanyia vitendo vya kihuni.
Akizungumza na Mtandao huu mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Juma Athuman alidai kwamba kijana huyo ana kawaida ya kuwateka watoto wadogo hasa wa shule na kuwapeleka chini ya daraja hilo na kuwafanyia vitendo vya kihuni.
" Kwa kipindi kirefu tulikuwa tukimsaka kibaka huyu ambaye ana tabia ya kuwateka watoto wadogo na kuwapeleka mto wa Morogoro chini ya daraja la Shani.
"Muda huu tumemfuma akiwa chini ya daraja hilo na mtoto mdogo ndipo tulipomfukuza na kufanikiwa kumkamata eneo hili la kituo cha mafuta jirani na daraja hili la Shani," alisema Juma Athuman.
Katika hatua nyingine 'ustadhi' mmoja alijitosa na kumnyakua kibaka huyo kutoka mikononi mwa kundi la wananchi hao na kumpeleka kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na eneo hilo la Shani SOURCE:
 

MATUKIO YA WANAFUNZI WA IFM WALIVYOCHEZEA KICHAPO KUTOKA KWA POLISI:



BAADA ya wanafunzi wa Chuo Cha Uongozi wa Fedha (IFM) kwenda kigamboni ambako Kamanda wa kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova kuwataka wakawasilishe hoja zao hukohuko ambako wanadai walipeleka majina ya wahalifu na hayajashughulikiwa, waligoma kufanya mkutano kwenye viwanja vya mpira eneo la Machava nakutaka mkutano huo ufanyike kwenye kituo cha polisi Cha Kigamboni ambako wanafunzi wengi wao walielekea huko.

VILIO NA KICHAPO TOKA KWA POLISI VILITAWALA MAANDAMANO YA YA WANAFUNZI WA IFM


Mwanafunzi aliyeshikwa akipandishwa kwenye Difenda.
Utakwenda Tu!


Mara baada ya kufika kwenye kituo hicho waliamriwa maratatu waondoke waende kwenye mkutano na Kamanda Kova wakakataa baada ya hapo ndipo mabomu yakaanza kupigwa. Kwenye mabomu hayo wanafunzi kadhaa walijeruhiwa na kuumia wengine walipoteza fahamu.

Hata hivyo walioshikiliwa wote waliachiwa na kutakiwa kwenda kwenye mkutano huo ambao uliazimia mambo kadhaa ya utekelezaji ili kutatua tatizo hilo la wizi kwenye eneo hilo. Kamanda Kova aliwaahidi wanafunzi hao kuwa watapata mrejesho wa hatua walizochukuwa siku ya tarehe 30 mwezi huu

Sunday, January 13, 2013

NEW TRACK-Gusher-Bado wewe

Kutana na Msanii Chipukizi "Gusher" anayekuja na crunk aloita "Bado wewe" ikiwa imewalenga viongozi walopotosha maana nzima ya uongozi bora nchini,Kijana Gusher toka panda za kaskazini mwa Tanzania amerekodi pini pande za noizmekah,ni mwenye juhudi na malengo makubwa katika kuonyesha kipaji chake anaomba support yenu mashabiki na wadau kwa ujumla, kupata kuisikiliza nyimbo hii ya "BADO

NEW TRACK-ManBatoo-She nah Leave(NOIZ)

Pata brand new riddim toka kwa ManBatoo aka Rudbwai from Arachuga Kijenge juu,Reggae joint inakwenda kwa jina "She nah leave" ikiwa ni new years release juu ya "heart & soul riddim" na mixing pande za www.noizmekah.com.

PSY-Gngnam Style Mash-Up

Thursday, January 10, 2013

Watu kumi na tatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma kwa tuhuma za mauaji yanayohusisha imani za kishirikina.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
 JESHI LA POLISI TANZANIA





YAH: TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA DODOMA KWA
 VYOMBO VYA HABARI TAREHE 10/01/2013.
Watu kumi na tatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi  Mkoani Dodoma kwa tuhuma za mauaji yanayohusisha imani za kishirikina.
Watu hao wanashikiliwa kutokana na tukio la mauaji lililotokea siku ya Jumatano tarehe 09/01/2013 majira ya saa 04:00 mchana katika kitongoji cha Mtakuja kata ya  Chitemo katika Wilaya ya Mpwapwa.
Katika tukio hilo  walisababisha kifo cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la NELSON S/O NYAGULU mwenye umri wa miaka 32, mkulima wa Chitemo  kwa kupigwa na risasi ya Bunduki aina ya Gobore tumboni na mtu aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KALANI.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba tarehe 08/01/2013 huko katika kijiji cha Chitemo kulikuwa na mnada, ambapo mvua ilinyesha sehemu moja ya kitongoji cha Mtakuja, sehemu ambayo alikuwa  anaishi mzee mmoja aliyejulikana kwa jina la LEONARD S/O NYAGALU, Miaka 70, Mgogo.
Kwa vile mvua hiyo haikunyesha sehemu kubwa katika kitongoji hicho inasemekana Mwenyekiti wa Kijiji JAVAN S/O MZAZI, Miaka 40, Mgogo, aliibua hoja kuwa kwa nini mvua inyeshe eneo moja tu analokaa Mzee huyo na kuacha kunyesha sehemu nyingine katika eneo hilo na kuwahamasisha wenzake kwenda kwa Mzee Nyagalu akawaeleze vizuri.
Majira ya 23.00 hrs usiku wakakusanyana na kuelekea kwa Mzee  Nyagalu, Walipofika Mzee huyo alisikia watu wakizungumza nyumbani kwake hivyo akavunja ukuta na akatoroka.
Inadaiwa kuwa kundi hilo lililokuwa limeongozana na Mwenyekiti wa Kijiji hicho waliingia ndani ya nyumba na kumkuta mke wa Mzee Leonard Nyagalu na kuanza kumpiga ili aonyeshe aliko mume wake, waliposhindwa kumpata wakabomoa nyumba na kuichoma moto.
Wakati wanafanya tukio hilo, walijitokeza watoto wa Mzee Leonard S/O Nyagalo, mmoja wao akiwa ni NELSON S/O NYAGALU, Miaka 32, Mgogo na ndipo nao wakaanza kupigwa.
Kwa mujibu wa watu walikuwa katika tukio hilo walisema ilisikika sauti ya mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la RASHID S/O KARANI akisema sasa mmetangaza vita na akafyatua gobore na risasi zikampata NELSON S/O NYAGALU tumboni zilizopelekea kupoteza maisha wakati anapata matibabu.
Baada ya kufyatua risasi toka katika gobole Bw. RASHID S/O KARANI aliwaaga wenzake kuwa anakwenda kujisalimisha Polisi lakini hadi sasa hajaonekana na jitihada za kumtafuta pamoja na silaha aliyotumia zinaendelea.
Majina ya wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na kushiriki katika tukio hilo  ni kama ifuatavyo:-
1.  Dickson S/O Chimosa, Miaka 52, Mgogo, Mkulima na Mkazi wa Chitemo.
2.  Javan S/O Mzazi, Miaka 44, Mgogo, Mwenyekiti wa Chitemo.
3.  Robert S/O Lusije, Miaka 51, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
4.  Donald S/O Mponi, Miaka 33, Mgogo, Mkulima na mkazi wa Chitemo.
5.  Daniel S/O Mwamba, Miaka 24, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
6.  Maneno S/O Ngaile, Miaka 36, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo
.
7.  Thomaso S/O Nyagalo, Miaka 28, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
8.  Gilbert S/O Lugaje, Miaka 39, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
9.  Aden S/O Simon, Miaka 33, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
10.      Malolo S/O Sanja, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
11.      Sospeter S/O Sanja, Miaka 35, Mgogo, Mkulima, Mkazi 
wa Chitemo.
12.      Jocktan S/O Chilomo, Miaka 40, Mgogo, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
13.      Keneth S/O Ngaile, Miaka 38, Mnyamwezi, Mkulima, Mkazi wa Chitemo.
Aidha siku ya Jumamosi tarehe 05/01/2013 majira ya 08:00 asubuhi kulikuwa na tukio la mauji  lililotokea katika Kitongoji cha Magungu, Kijiji cha Mpendo, Kata ya Mpendo Tarafa ya Kwa Mtoro Wilaya ya Chemba Mkoa wa Dodoma.
Ambapo mtoto mmoja aliyetambulika kwa jina la TONY S/O SOKOINE mwenye umri wa miaka miwili na nusu (2.5), mkazi wa Kijiji cha Mpendo alifariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa kuchomwa na kisu shingoni kilichorushwa na mtoto mwenzake aliyefahamika kwa jina la SOMEI S/O REMENDA mwenye umri wa miaka mine (4) mkazi wa Kijiji cha Mpendo.
Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha Kifo hicho ni kwamba marehemu na mtuhumiwa walikuwa wanacheza nje nyumbani kwao kwa akina SOKOINE S/O RENENDA ambapo mtuhumiwa alirusha kisu kwa lengo la kumuua ndege aliyekuwa juu ya mti  uliokuwa karibu na nyumba yao, ndipo kisu huchi kiligonga kwenye mti huo na wakati kinadondoka kilimjeruhi marehemu kwa kumchoma shingoni  na kusababisha kifo chake.
 
DAVID A. MISIME - ACP
                  KAMANDA WA POLISI MKOA WA DODOMA    

YOU’RE MORE IMPORTANT


YOURE MORE IMPORTANT
          Man is a social being; he interacts with many people from different areas.
           Looking around at where I am I see people, so many. Some I know some I know some I don’t; just different people. Looking at them closely I see one thing; they are all different; so are their thoughts, beliefs, goals and ideas. Each one has his or her self values and needs.
           But life is for living, living is interacting with these different people; every hour, every minute and every second. If you interact with them they have access to your life. Everyone wants to make you be how they want you to be. But the question is how should you be to please all those around you? Who should you listen to as to please all of them?
           Trying to please all of them is impossible; it is very far from being possible. Be yourself that’s the only way out. You are more important than anyone else around you. They can only advice but the effects of whatever they advice come directly to you; not to all those around you, no matter how close they are. Only you suffer the blow of what you do.
             I once asked myself; why didn’t God put only one brain so that we can all share it? Why do we get hurt individually and all together? Why?
What others want for you is not important for you, that is what they want not what God wants for you; not the reason why you were created, what you want for you is very important. It’s your mission in your life. It leads to your destination;                        YOUR DESTINATION, no one else YOURS ONLY.
             No one else has the power to make you fail unless you allow them to do so. We open the doors of our lives to them and they penetrate too much that we can’t even stand on what we want. What do we get when we fulfill the dreams of the world to us and fail to achieve our own goals.
              You have the powers to decide the extent to which people can interfere with your life and way of living. In your life you’re more important. Oxygen is for all of us but you breathe through your own nose; not through anyone’s nose; that shows in life you stand alone!
It is your fight not a TEAM WORK. You’re responsible for your life!!!
      Prepared by HEAVEN DAVID

PICHA YA AJALI ILITOKEA JANA,BASI LA BUNDA EXPRESS

Eneo la katikati ya Lugeye na Nyanguge basi la abiria la 'Bunda Express' lenye namba za usajili T 782 BKZ likitokea Musoma kuelekea Mwanza muda wa saa mbili asubuhi jana lilipata ajali mbaya, mazingira yanaonesha kuwa idadi kubwa ya watu wamekutwa na umauti na wengine kuwa majeruhi na mvua kubwa ilikuwa ikinyesha.
Eneo la magu basi la abiria la 'Bunda Express' lenye namba za usajili T 782 BKZ likitokea Musoma kuelekea Mwanza muda wa saa mbili asubuhi jana lilipata ajali mbaya, mazingira yanaonesha kuwa idadi kubwa ya watu wamekutwa na umauti na wengine kuwa majeruhi na mvua kubwa ilikuwa ikinyesha.

Tuesday, January 1, 2013

Make 2013 better to avoid past mistakes




As Tanzanians today bid goodbye to year 2012 and happy new year 2013, they look forward to yet another eventful year ahead that starts today.
                 Last year was bad for many people, what withit being ushered in by such calamities as the Msimbazi river floods in December- January in Dar es Salaam that left thousands of people homeless up to now.
                Then there were bombs that exploded fromarmy depots camps at Gongo la Mboto which had devastating effects on neighbourhoodresidents.
                  There were, furthermore, ghastly road accidents that led to loss of life and limb for many passengers, and religious skirmishes in both Mainland Tanzania and Zanzibar. As they year 2013 unfolds,Tanzanians shouldreflect on shortcomings and chart the best way forward. Army camps, for instance, shouldbe located at distances far away from wananchi, to avoid disasters like Mbagala’s and Gongo la Mboto’s.
                We understand that when they were first set upthey were in remote areas that were inaccessible to members of the public.But, as the population grew, people slowly started to move near them, what with the army being the people’s defence force. Slowly people built makeshift structures and later permanent ones, finding in soldiers a ready market for selling food and other items.
But the authorities concerned were unwittingly courting disaster.Be that as it may, however, we find it odd that there are people still living in tents at Mabwepande where survivors of floods along Msimbazi River were shifted to, a year on.
As for traffic accidents, much has been said, but it needs the will of everybody concerned to keep them to the barest minimum.
            These include the traffic police, drivers, Surface and Marine Transport Authority (Sumatra), Tanzania Roads Agency (Tanroads), legislators and law courts.
They should crack their heads to find solutions to the problem of recurring road accidents, and not only issue orders from the comfort of their air-conditioned offices.

Kifaa cha Tablet kutoka Afrika


Kifaa cha Tablet
Kifaa cha Tablet kilichoundwa barani Afrika

Simu aina ya smartphone na kompyuta za tablet zinazosemekana kuwa vifaa vya mawasiliano vya kwanza kutengenezwa na kampuni ya Afrika zimezinduliwa.
Vifaa hivyo, ambavyo vimebuniwa na mjasiriamali wa Congo,vinatengenezwa nchini China.
Kampuni yake ya VMK, vifaa vyake vinaendeshwa kwa teknolojia ya Android ya Googles.

Simu hizo za smartphone zitauzwa kwa bei ya rejareja ya dola $170, sawa na pauni za Uingereza (£105) na kompyuta itauzwa kwa dola $300 sawa na pauni (£185).
"Ni Waafrika wenyewe, ndiyo watakaofahamu mahitaji ya Afrika," amesema Bwana Mankou katika mkutano wa Tech4Africa mjini Johannesburg.
"Apple ni kampuni kubwa Marekani, Samsung ni barani Asia na tunataka VMK kuwa kampuni kubwa barani Afrika."

Kifaa cha Tablet kilichoundwa barani Afrika
Blogu ya teknolojia ya Smartplanet imeripoti kuwa kompyuta za VMK zinatoa huduma ya uunganishaji wa wi-fi na uwezo wa gigabytes 4 ambazo zimehifadhiwa ndani yake.
Jina lake, Way-C, lina maana ya "mwanga wa nyota" katika lugha ya Kilingala.
Simu hiyo ya smartphone nyuma na mbele ina kamera na skrini ya ukubwa wa inchi 3.5 sawa na sentimita 8.9.
Verone Mankou
Verone Mankou, ndiye aliyeunda kifaa hiki
Kuna mipango ya kuuza simu hizi katika nchi kumi za Afrika Magharibi pamoja na Ubelhiji, Ufaransa na India.
Bwana Mankou amesema anatarajia kuzindua uuzaji wa kompyuta za bei nafuu zaidi kwa wanafunzi mwaka ujao.
VMK imesisitiza kuwa wakati bidhaa zake zinatengenezwa China kwa sababu za unafuu wa gharama, ubunifu na uhandisi wa simu hizo ni wa Kiafrika.
Hii ni kutokana na baadhi ya watu au kampuni za biashara kupinga uwezo wa kampuni hiyo katika teknolojia ya simu na kompyuta.

Kampuni ya VMK imesema kinyume na bidhaa nyingine za awali za simu na komputa zilizosemekana kuwa za Afrika, bidhaa za VMK hazifanani na bidhaa zozote za aina hiyo katika nchi nyingine.
source:BBC

HUYU NDIO DADA YAKE MARIO BALOTELLI AMBAE YUKO MAPENZINI NA MCHEZAJI OBAFEMI MARTIN.


.
Kwa wiki kadhaa sasa hivi zimekuwepo taarifa kwamba mchezaji wa Manchester City Mario Balotelli amekasirishwa na kitendo cha mchezaji wa Nigeria Obafemi Martins kuingia kwenye mapenzi mazito na dada yake, yani dada wa Balotelli.
Obafemi ameamua kuzungumza kwa kusisitiza kwamba hizo ni habari tu kwamba Mario kakasirika lakini sio kweli, Balotelli anafurahi dada yake kuwa mapenzini na Obafemi.

Wapenzi hawa wamekua wakionekana sehemu mbalimbali za goodtimes na wameonekana wazi kabisa kuwa kwenye mapenzi mazito.
Obafemi amekaririwa na Daily Post akisisitiza kwamba “Mario ni mshkaji wangu, ananiheshimu na mimi namuheshimu… habari za yeye kukasirika ni watu tu wanatunga”


Balotelli
Obafemi amesema ni kweli yuko kwenye mapenzi mazito na Abigail lakini hawana mpango wa kuoana sasa hivi na wala hawajawahi kuliongelea hilo.
Kwenye interview na gazeti la The Sun April 2012 Abigail ambae ni dada wa Mario Balotelli alisisitiza kwamba hana mpango wa kuwa mapenzini na mchezaji yeyote wa mpira kwa sababu ni watu wanaozungukwa sana na wasichana, wasichana wanajipeleka wenyewe bila kuitwa, hata Balotelli hatomruhusu kuwa na mpenzi mwanasoka lakini naona mambo yamekua tofauti sasa hiv

ASKARI ALIYEPIGA PICHA NA LEMA ATOROKA JESHINI


JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema askari anayedaiwa kuwa jeshi hilo aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ametoroka.
 
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema jana kwamba pamoja na hatua yake ya kutoroka, jeshi litaendelea kumsaka kwa udi na uvumba ili kumhoji na kujiridhisha kama kweli ni mwanajeshi wake kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kifungu cha 147 cha Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya 1977.
 
“Huyu kijana inasemekana alishawahi kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), lakini wakati tunaendelea na uchunguzi alitoroka katika nyumba aliyokuwa amepanga bila ya taarifa kwa baba mwenye nyumba,” alisema Kanali Mgawe na kuongeza:
 
“Askari huyo alikuwa anaishi katika nyumba ya kupanga mita chache karibu na Kituo cha Polisi cha Simanjiro, Arusha na alikuwa akijishirikisha na ulinzi shirikishi.”
 
Alipoulizwa jina la askari huyo, Kanali Mgawe alijibu: “Yeye alikuwa anafahamika mtaani hapo kwa jina la kamanda.”
 
Hata hivyo, Kanali Mgawe alisema jeshi hilo litahakikisha linatoa ripoti kamili kwa umma baada ya kumkamata na uchunguzi kukamilika ili kuondoa utata uliogubika suala hilo.

Alipoulizwa kama kuna tofauti gani kati ya mwanajeshi kuingia kwenye mikutano ya wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kisiasa kama wakuu wa wilaya na mikoa, Kanali Mgawe alijibu:” Wanajeshi wanaofanya kazi za U-DC au RC, wanaruhusiwa kisheria.”
 
Alifafanua kuwa iwapo mwanajeshi atateuliwa kufanya kazi katika taasisi yeyote ya Serikali nje ya jeshi, atatakiwa kuvua magwanda ya jeshi na kufanya kazi hiyo mpaka atakapomaliza muda wake na baada ya hapo ataruhusiwa kurejea jeshini.
 
“Kuna kitu kinaitwa ‘secondment.’ Mwanajeshi anaruhusiwa kufanya shughuli zozote nje ya jeshi iwapo atahitajika kufanya hivyo. Ila kwa masharti ya kuvua magwanda, hivyo wananchi wasishangae kuwaona baadhi ya askari wetu ni wakuu wa wilaya na mikoa na baadaye kurudi jeshini kuendelea na majukumu yao,” alisema Kanali Mgawe na kuongeza:
 
“Askari akiwa katika majukumu yake mapya, atafanya kazi zote atakazopewa zikiwamo za kisiasa kama ilivyo kwa wakuu wa wilaya na mikoa, lakini akirudi jeshini, anarudi kuwa askari mwenye utii na kufuata kanuni za jeshi zisizofungamana na siasa.”

RIPOTI FUPI YA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI- TANZANIA


Matokeo rasmi ya sensa yametoka. Idadi ya Watanzania ni milioni arobaini na nne nukta tisa. (44.9million).


Matokeo hayo yametangazwa leo katika viwanja vya Mnazimmoja jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.

Jumla: 44,929,002. TZ Bara 43,625,434 na Zanzibar 1,303,568
Source:MPEKUZI

MAJUU WAKISHANGILIA MWAKA MPYA WABONGO TUNASHEHEREAJE

 New Year's Eve celebrations around the world hapa Pakistan Rob Crilly... ukiwa mji umenuka mbaya kwa shagwe!!!


 Hapa watu wakiwa wanasherekeea kwa kuangalia  fireworks are lighting up the city's skyline



Australia welcomes in the New Year
• Revellers around the world prepare to celebrate the start of 2013
• India's army cancels New Year celebrations in remembrance of gang-rape victim
• Britain expects washout New Year as flooding countinues
• Record turnout expected for Hogmanay in Edinburgh