Tuesday, January 22, 2013

SAKATA LA KAHABA ALIYEOKOKA......


Hili ni simulizi la  kweli linalomhusu mwanamke  mmoja ambaye alikuwa ni kahaba  wa makahaba......
Mwanamke  huyu  alijitambua  vyema  na  kukiri  ndani ya  nafsi yake kuwa hawezi  kuolewa  na mwanaume  yoyote  yule  maana  jamii yote ilikuwa inamtambua  kwa uchangudoa  wake......

Kwa hiyo , ili kurahisisha mambo na  kuifanya  biashara  yake  iimarike, mwanadada  huyu aliamua  kwenda hospitali kukitoa  kizazi chake.Hakutaka  tena  usumbufu wa kutoa  mimba  au kufikiria kondomu......

Tangu wakati  ule biashara  yake  iliimarika na wateja  walizidi kumiminika.Baada  ya miaka  kadhaa, Upako  wa  mwenyezi mungu  ulimfikia kupitia kwa mtumishi  mmoja  wa  mungu ambaye  alifanikiwa  kumfanya  aokoke  na  kuwa mtumishi mzuri  kanisani.....
 
Siku moja, mchungaji  mmoja alimwita na  kumwambia  kuwa:
"Dada yangu, Mwenyezi mungu  amenena  na  mimi na  kunifunulia  kuwa  wewe  ndo mke  wangu wa ndoa, hivyo naomba tuoane.."

Mwanamke huyu alitabasamu na kusema:
 "Kaka  yangu, Mungu hajakwambia lolote, lasivyo, utakuwa  hujamsikia vizuri.Naomba  uniache tu maana  sina  mpango wowote wa  kuolewa"

Yule  mchungaji  aliendelea kushikilia  msimamo wake  na  kudai kuwa :

"Mungu  amenifunulia,wewe  ndo  mke wangu" 

Mwanamke  huyu  aliendelea  kuyapuuza  maneno hayo na ndipo sakata  hilo  lilipomfikia  Askofu  wa  kanisa  hilo.....

Wakiwa mbele  ya mchungaji,Mwanamke huyu  alifunguka  kwa  uwazi mbele  ya askofu  na  kudai kuwa kabla ya kuokoka yeye  alikuwa  ni kahaba  wa  makahaba....

Askofu naye alifunguka  na  kudai kuwa :"Sioni sababu ya kuumiza kichwa  kwa  mambo yaliyopita.Mungu  humsamehe  mwanadamu  kwa  kuzifuta  dhambi zake  zote za  nyuma  na  kumfanya  awe  mpya..!!!"

Mwanamke huyu  alifunguka  tena na kudai kuwa:
"Baba  askofu, mimi  nilishatoa kizazi changu  wakati nikiwa  kahaba, kwa hiyo  sitaweza    kuzaa  tena"
Askofu  aliishiwa  pumzi baada  ya kusikia hivyo.Hakuweza tena  kusema  kuhusu  kusahau ya  nyuma.Ilibidi amgeukie yule mchungaji  na  kumwamba: 

"Vipi, bado  kuna maono yoyote  toka  kwa mwenyezi mungu?" 

Mchungaji alijibu  ,"Ndio, huyu ndo mke wangu.."

 Askofu  ilibidi  awaombee kwa  sala  maalumu.Hatimaye ndoa  ikafungwa......Baada  ya  miezi  michachtu, huyu mwanamke  alibeba  mimba.Yeye  pamoja  na mumewe waliongozana pamoja kwenda  hospitalini, tena  kwa  yule  yule doctor  aliyekitoa  kile  kizazi......

Daktari  alipomuona  alifurahi  akidhani kuwa pengine  mteja  wake  kamletea  mteja mwingine.....Doctor  hakuamini  masikio  yake baada  ya kuambiwa kuwa  huyu  mwanamke ni mjamzito na  amekuja  kujiandikisha  clinic....
Hakika Mungu ni  Muweza wa  yote.... 
SOURCE;MPEKUZI 

MWANACHUO WA SAINT JOHN, DODOMA AUAWA KIKATILI

JESHI la polisi mkoani Dodoma limeshutumiwa kwa kushindwa kuimarisha ulinzi katika baadhi ya maeneo mkoani humo hatua inayodaiwa kuchangia kuaawa kinyama kwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Saint John Lidya Leo Mzima na watu wasiojulikana.

Marehemu Lidya mwenye umri wa miaka 57 anadaiwa kuuawa siku ya jumapili hii majira ya saa nne za usiku pembezoni mwa maeneo ya chuo hicho chenye wanafunzi 5500
akiwa anarejea nyumbani baada ya masomo ya jioni.

Ni simanzi,vilio,huzuni na majonzi katika vyunga vya chuo hiki kufuatia tukio hili la kusikitisha ambalo linadaiwa kuyaweka katika mashaka na wasiwasi mkubwa maisha ya wanafunzi hawa.


Licha ya kulitupia lawama jeshi la polisi baadhi ya mashuhuda wanadai kuwa baada ya kufikwa na mkasa huo uliositisha safari ya maisha yake mwili wa marehemu Lidya uliharibiwa vibaya na mnyama asiyejulikana kwa kunyofolewa macho,masikio,pua,mguu na viuno vingine.


Prof.Gabriel Mwaluko ni makamu mkuu wa Chuo na Karimu Meshack ni afisa habari ambao kwa pamoja wanaelezea kilichorjiri.


Kutokana na shutuma za uzembe dhidi ya jeshi hilo, Kamanda wa mkoa ACP David Misime anawataka wakazi wa mkoa huo kuimarisha ulinzi shirikishi kwa lengo la kuwabaini wahalifu.


Wakati huo huo Kamanda Misime anasema msako mkali umeanza wa kuwatia nguvuni waliohusika na ukatili huo ili waweze kufikishwa kwenye mikono ya sheria kwa ajili ya hukumu.

Monday, January 21, 2013

RAIS BARACK ABAMA AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA MAREKANI KWA KIPINDI CHA PILI



Rais Barack Obama aliapishwa rasmi  Jumapili kuongoza Marekani kwa muhula wa pili wa miaka minne. Makamu rais wake Joe Biden pia aliapishwa.

Tukio hilo muhimu litafanywa tena kwenye sherehe za leo Jumatatu ambazo zinategemewa kushuhudiwa na maelfu ya watu katika uwanja mkuu  wa kitaifa hapa jijini Washington DC.

Bwana Obama alikula kiapo saa chache kabla ya saa sita mchana Jumapili akiwa White House katika sherehe zilizochukua  nusu dakika akiwa katika chumba cha  Blu. 

Akiwa na mkewe Michele Obama na binti zake Malia na Sasha na kundi ndogo la waandishi habari, jaji mkuu John Roberts alimwapisha rais Obama kwa muhula wa pili.

Baada ya kula kiapo rais Obama alisalimiana na jaji huyo, na kuwapa  busu mkewe na binti zake, akiwaambia, “nimefanya hivyo”.

Hii ni mara ya saba katika historia ya Marekani kwa rais kula kiapo Jumapili kabla ya sherehe za umma Jumatatu inayofuata. Katiba ya Marekani inasema wazi kuwa muhula wa rais sharti uanze rasmi Januari 20 .

Bw. Obama alitumia Biblia iliyokuwa ya nyanya ya mkewe, LaVaughn Delores Robinson kula kiapo.Katika sherehe za umma baadaye leo Jumatatu nje ya majengo ya bunge, kwa mara nyingine tena atawekelea mikono yake kwenye Biblia iliyotumiwa na rais Abraham Lincoln alipoapishwa mwaka wa 1861. Bwana Obama atatumia Biblia ya pili, iliyomilikiwa na mtetezi wa haki za kiraia Martin Luther King Jr.

Sherehe za leo Jumatatu zitafanyika sambamba na siku kuu ya kitaifa ya Martin Luther King Jr. Mapema Jumapili, rais Obama na familia yake walihudhuria ibada katika kanisa la Metropolitan African Methodist Episcopal Church.

Naye makamu rais Joe Biden  alikula kiapo cha kuhudumu muhula wa pili  katika makao yake rasmi  ya Naval Observatory hapa jijini Washington akitumia Biblia ya familia. 

Aliapishwa na jaji wa mahakama kuu Sonia Sotomayor  na hii ni mara ya kwanza kwa jaji mwenye asili ya kihispania kumwapisha makamu rais wa Marekani.

Rais Obama anaanza muhula wake wa pili huku Wamarekani wakiwa na hisia mchanganyiko kuhusu hali ya kiuchumi, na uwezo wa viongozi wa vyama vyote viwili kuondoa tofauti zao za kisiasa na kutoa kipaumbele katika maswala ya kuongeza ajira na kutatua matatizo ya  kifedha.  Kauli mbiu ya  rais Obama anapoapishwa kwa muhula wa pili ni ; “watu wetu,hali yetu ya baadaye.”

Wiki jana Ikulu ya White House ilitoa video ikiwa na ujumbe wa rais Obama akisema “nchi hii imepitia kipindi kigumu, lakini hatimaye tunaibuka tukiwa na nguvu zaidi“  tunaendelea kuimarisha muungano wetu kuhakikisha kila mtu anapata haki yake endapo atafanya bidii bila kujali anakotokea.”

UKUTA WA KITUO CHA MABASI UBUNGO WANGUKIA MAGARI YANAYOKADIRIWA KUFIKIA 24 LEO HII:

 Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.
 Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.
 Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.
 Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.
 Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.
 Watu wakiangalia magari yao.
 Kenyela akiongea jambo juu ya ajali hiyo.
 likuwa ni hasara tupu.

SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo alfajiri  umeanguka na kuyaharibu vibaya magari  zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa nje ya eneo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.

Sunday, January 20, 2013

SAKATA LA GESI: MTWARA NI MABOMU NA RISASI ZA MOTO....



MABOMU na risasi za moto jana zilitawala katika mji wa Mtwara na vitongoji vyake baada ya wananchi kufanya maandamano makubwa kupinga ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kwenda Dar es Salaam.
 
Maandamano hayo yaliandaliwa na Chama Cha Wananchi (CUF) na kuongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa Bara, Julius Mtatiro, ambaye alifuatana na wabunge wa chama hicho wanaotoka mikoa ya kusini.

Maandamano hayo yamefanyika baada ya maandamano mengine makubwa yaliyofanyika Desemba 27 mwaka jana kwa lengo hilohilo, yakiwa yamendaliwa na vyama vinane vya siasa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka mkoani humo, maandamano ya jana yalifanyika huku wanawake wakiwa mstari wa mbele.
Chanzo cha kupigwa mabomu hayo kinaelezwa kuwa ni kukatika kwa umeme katika eneo ulikokuwa unafanyika mkutano wa hadhara wa CUF ambako wananchi waliahamaki na kuandamana kwenda ofisi za Tanesco Mtwara i kujua chanzo kukatika kwake.

Wakiwa njiani kuelekea Tanesco umati huo mkubwa wa wafuasi wa CUF ulikutana na Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) ambao waliamua kuwatawanya kwa mabomu na kupiga risasi za moto hewani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mtatiro jana, lengo la kufanya maandamano na mkutano huo lilikuwa ni kupokea karatasi ya kupinga ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam
Alisema akiwa katika mkutano huo alipokea saini 10,000 za wananchi wa mikoa ya kusini ambao wanapinga mpango huo wa serikali kuisafirisha gesi. 

Maandamano hayo yalihitimishwa na mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Mashujaa mjini Mtwara na wabunge wa CUF waliokuwapo ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tabora, Magdalena Sakaya (Tabora), Mbunge wa Mkanyageni Habib Mnyaa, Salum Barwan (Lindi Mjini), Said Bungara "Bwege" Kilwa Kusini na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mtwara, Clara Mwituka.

Mtatiro alisema msingi wa hoja yao ni kujikita katika kuhakikisha gesi inatumika kwa faida ya taifa lakini kwa kutoa kipaumbele katika maeneo yaliyo nyuma katika maendeleo, kama kusini.


Watu wakamatwa mitaani

Kutokana na vurugu hizo inaelezwa kuwa zaidi ya watu 20 walitiwa mbaroni na jeshi la polisi. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Mary Nzuki hakuweza kupatikana jana kwa simu yake ya kiganjani. 

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Mtwara, Tutufye Mwakagamba alikiri kukamatwa kwa watu kadhaa katika vurugu hizo ingawa alimtaka mwandishi wa habari hizi amtafute baadaye.


“Ni kweli ndugu yangu kuna watu kadhaa tumewakamata katika vurugu zilizotokea leo (jana), lakini ninakuomba nitafute baadaye kwa sababu muda huu nipo katika mkutano wa CUF ambako kuna mvua kubwa inanyesha,” alisema Kamanda Mwakagamba.

Biashara zafungwa
Kutokana na maandamano hayo yaliyoambatana na vurugu biashara mbalimbali zilifungwa katika soko kuu la Mtwara na mitaani hali iliyowafanya wananchi kuwa katika wakati mgumu.

Magari ya CUF kila kona
Habari zinasema mkutano wa jana ulikuwa na shamrashara za aina yake na zaidi ya magari 14 yalisafirisha wafuasi wa CUF kutoka wilayani Tandahimba wakati magari mengine manane yalitokea wilayani Newala.

Wakati huohuo, Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile (CCM), ameibuka na kuitaka serikali kutodharau madai ya wananchi wa mikoa ya kusini kuhusu suala la gesi.

Aliyasema hayo wiki chache baada ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara kufanya maandamano ya amani kupinga ujenzi wa bomba la kusarisha gesi kutoka mkoani humo kwenda Dar es Salaam.

Dk. Ndugulile, alisema kwa mtazamo wake suala hilo lina sura mbili tofauti ambayo yote yana hoja za msingi ikiwamo umaskini wa mikoa ya kusini na tataizo la ajira kwa vijana

YANGA YAIBUTUA BLACK LEOPARD 3-2 ,TEGETE ATUPIA MBILI CHEKI PICHA:

5 


7 
Wachrezaji wa timu ya Yanga wakishangilia mara baada ya kufunga goli la kwanza katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.
1  
Mashabiki wa Yanga wakishangilia wakati timu yao ikicheza kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
2 
Kikosi cha timu ya Yanga kikiwa katika picha ya pamoja.
Mchezaji wa timu ya Yanga Kabange Twite akimiliki mpira mbele ya Nkosiabo  Xakane mchezaji wa Black Leopards ya Afrika Kusini  .katika mchezo wa kirafiki uliokutanisha timu hizo kwenye uwanja wa Taifa jioni hii, timu ya Yanga imeshinda magoli 3-2 dhidi ya timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini.
Goli la Yanga limefungwa na mchezaji Jerrison Tegete kwa penati katika kipindi cha kwanza baada ya Mchezaji Haruna Niyonzima kuangushwa katika eneo la hatari na mchezaji wa timu ya Black Leopards na kuongeza goli la tatu katika kipindi cha pili , Huku mchezaji Didier Kavumbagu akapachika goli la pili katika kipindi katika kipindi hichohicho cha pili cha mchezo.
Timu ya Black Leopards ya Afrika Kusini imefanikiwa kupata magoli mawili katika kipindi cha pili na kufanya matokeo kuwa Yanga 3 na timu ya Black Leopards 2 mpaka mwisho wa mchezao huo.

Dr Slaa alipua bomu




















Adai serikali imeagiza mtambo wa kuhujumu mawasiliano ya wapinzani

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa amebaini kuwapo mpango wa serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuingiza mtambo wa kuingilia mawasiliano ya wapinzani kwa ajili ya kuhujumu uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Dk. Slaa ambaye ni mara yake ya pili kutoa tuhuma za CCM kuingiza mtambo wa kuingilia mawasiliano ya CHADEMA, alisema tayari ameshapata e-mail yenye kuonyesha thamani ya mtambo huo na kwamba utagharimu dola 850,000 za Marekani, karibu sawa na sh bil. 1.3.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua kongamano la vijana wa vyuo vikuu wa CHADEMA (Chaso), jijini Dar es Salaam, lililokuwa na lengo la kujitathmini na kupanga mikakati ya kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015 pamoja na kuwaapisha viongozi wapya wa shirikisho hilo.
Alisema tayari ameshaandika barua kwa mamlaka husika kuwajulisha hilo, lakini hadi sasa hawajajibu.
“Tuna ‘details’ na nyaraka nyingi zinazoonesha namna mtambo utakavyotumika kwa ajili ya kuwahujumu wapinzani na kwa kuwa tumeshaandika barua kwa mamlaka husika na hawajatujibu, kwa sasa sitaenda kwa undani zaidi juu ya hili. Subirini siku ifike nitaweka kila kitu hadharani,” alisema Dk. Slaa.
Alisema CCM kwa kushirikiana na Idara ya Usalama wa Taifa, wamekuwa wakitengeneza propaganda mbalimbali za kutaka kumchafua yeye pamoja na CHADEMA, lengo likiwa kuwaondoa Watanzania katika ajenda za msingi za kupigania ukombozi.
Aliongeza kuwa, awali mahasimu wake kisiasa walikuja na propaganda kuwa amechukua mke wa mtu, kisha wakasema amedhulumu viwanja huko Mabwepande na sasa wameanzisha suala la kukopa sh milioni 140 ambalo alifafanua kwamba halina ukweli wowote.
“Wanawalisha maneno wale wanaokubali kununulika, msifikiri yale yanatoka midomoni mwao hapana, lakini watambue leo hakuna Mtanzania atakayehangaika na uongo unaotengenezwa kwa ajili ya kuwafanya wazidi kutawaliwa,” alisema Dk. Slaa.
Akizungumzia tuhuma za CCM na serikali kushirikiana kuingiza mtambo wa kuhujumu mawasiliano ya wapinzani, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye alisema madai hayo ni ya uongo.
Akizungumzia vita dhidi ya ufisadi nchini Dk Slaa, alisema wanaojidanganya kwa kusema kwamba kwa sasa siyo agenda ya Watanzania, wamefilisika kimawazo kwa kuwa suala hilo halitanyamaziwa na CHADEMA mpaka wahusika watakapotiwa mbaroni.
“Kama wanataka tunyamaze kuhusu ufisadi basi waturudishie twiga waliowatorosha, fedha za EPA, mabilioni ya Uswisi na pia watuambie ni kina nani wanawaua tembo walio katika hifadhi zetu na kisha kusafirisha pembe kupitia bandari zinazolindwa na watu wanaolipwa kwa kodi za Watanzania… vinginevyo hakuna wa kutunyamazisha zaidi ya Mwenyezi Mungu,” alisema Dk. Slaa.
Akielezea sera ya majimbo na mafanikio ya mikutano ya chama hicho kwa mwaka 2012, Dk. Slaa, alisema imekuwa na mafanikio makubwa hasa baada ya wananchi kuzinduka na kuamua kudai haki za kutaka kunufaishwa na rasilimali zinazowazunguka.
Alisema miaka minane iliyopita wakati CHADEMA waliposema rasilimali za nchi zianze kunufaisha eneo husika kwanza, watu wengi hawakuelewa, lakini leo baada ya kufikiwa na ufahamu kupitia Operersheni za CHADEMA, maarufu kwa jina la M4C, kila eneo limezinduka na sasa serikali inaanza kuwaona watu hao kuwa maadui kwa kuwa wanadai kuthaminiwa.
“Nchi yetu kila eneo kuna rasilimali na hatusemi ziwanufaishe watu wa eneo husika tu, bali tunataka waanze wao na ziada ndiyo iende maeneo mengine, leo mnawaona Mtwara na Lindi wanapigania haki hiyo na maeneo mengine hivyo hivyo, kwa hiyo tuna haki ya kujivunia mafanikio ya kuwaelewesha wananchi juu ya kudai haki zao,” alisema Dk. Slaa.
Aliongeza kuwa, mwaka huu watahakikisha suala la mauaji holela ya raia wasio na hatia, halijirudii ikiwa ni pamoja na kuishinikiza serikali iunde tume huru ya kimahakama kufuatilia matukio yote ya mauaji yenye utata yanayohusishwa na harakati za kisiasa mwaka 2012.
Akizungumzia suala la kufukuzana ndani ya CHADEMA, Dk Slaa alisema hawataogopa kumfukuza mwanachama yeyote msaliti anayeenda kinyume na katiba ya chama hicho na kutolea mfano madiwani waliofukuzwa mkoani Arusha na wanachama wengine.
Alisema licha ya madiwani wa Arusha kujua walifukuzwa kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA, waliamua kwenda mahakamani kutaka kukisumbua chama, hali aliyosema mahakama haikuweza kukubaliana nao na sasa wanawajibika kulipa gharama za kesi na wakishindwa wataenda gerezani.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, aliitaka CCM imshauri Rais Jakaya Kikwete aunde tume huru kuchunguza mauaji mbalimbali ya kisiasa yanayotokea nchini badala ya kupanda jukwaani na kusema CHADEMA ndio wauaji.
Alisema kuwa kila siku Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba na viongozi wengine ndani ya chama chao wamekuwa wakitaka kuwaaminisha wananchi kuwa CHADEMA inahusika na mauaji ya kisiasa.
“Nape anasema CHADEMA wanahusika na mauaji ya kisiasa, Mwigulu naye hivyo hivyo, viongozi wengine ndani ya chama chao nao wanapiga kelele hizo hizo, sisi CHADEMA tunasema iundwe tume huru ya kimahakama wao wanaogopa, wanajua wataumbuka juu ya ufedhuli wao,” alisema Mnyika.
Aidha, alisema wamebaini CCM inachapisha kadi za CHADEMA na kisha kuwagawia wanachama wao ili kuwahadaa wananchi kuwa chama hichi kinakimbiwa.
“Unajua ukiona mtu anajidanganya mwenyewe, huyo inabidi umsikitikie kwa kuwa kila njia ya udanganyifu wao sasa imeshabainika katika mioyo ya Watanzania, na sasa wameona wajaribu kujiridhisha katika nafsi zao wakiwa katika mikutano ya hadhara kwa kupeana kadi walizochapisha wenyewe huku wakishangiliana,” alisema Mnyika.


source:tanzania daima

Saturday, January 19, 2013

PAPARAZ.COM COMEDY TV SHOW COMING SOON


PAPARAZ . COM COMEDY TV SHOW COMING SOON..............
Hii ni comedy iliyoandaliwa kwa umahiri  wa hali ya juu,ambayo itakuja kuwashika watazamaji wote wa TBC 1, ikiwa imeandaliwa na MAC MEDIA  ni komedi inayohusu maisha ya Mtanzania ambayo yanafuatiliwa pasipo MTANZANIA kujua kuwa yanafuatiliwa.
        Kama ilivyozoeleka neno Paparaz linamaanisha mpiga picha mahiri anayepiga picha kwa watu au mahali fulani kwa kujificha,picha hizo huwa ni bora kwani zinaoonesha maisha halisi ya mtu akiwa amejiachia.
          Comedy show hii itakuonesha maisha ya Watanzania wakiwa wamejiachia,utaburudika na kuvunja mbavu kutokana na mambo yaliyomo katika serious comedy hii.

ITAANZA LINI ?
Comedy hii itaanza mwishoni mwa mwezi huu wa kwanza

WAPI ? 
    TBC 1
   
!!!!!!!!!!!!!!!!!!     ITAKAPOANZA KURUSHWA DONT MISS TAFADHALI   !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!    

Teaser: Kaa tayari kwa video ya 'Ki-utu Uzima' by Joh Makini...Coming soon.

Mwamba wa kaskazini mweusi Joh Makini ametoa ishara, soon atawasha 'green light'. Kaa tayari kuipokea video yake mpya ya Ki-Utu Uzima, cooming soon.

Teaser: Mwana Fa - The Finest


Mwana Fa a.k.a Binamu ametease picha hii kupitia akaunti yake ya Instagram, so ni miongoni mwa new joints zinazotegemewa kutoka hivi karibuni.

NEW TRACK : AINEA ft SHETA - SOMEBODY

                                PROUCTION : ECK PRODUCTION
                                PRODUCER :   ECK

LISTEN -Belle 9 - (Official Music Video)

Friday, January 18, 2013

NEW TRACK : JACO BEATS - LOVE IS


                                          SONG : LOVE IS
                                          MSANII : JACO BEATS
                                          PRODUCTION : LONG MILES
                                          PRODUCER : JACO BEATS
   Jaco Beats ni moja ya wasanii wanaofanya vizuri katika industry ya mziki Tanzania. Anafanya vizuri akiwa msanii huku Producer,Mziki wake anaufanya pande za Dodoma.
 

Wednesday, January 16, 2013

New Song: Pnc, Z-Anto, Dogo Janja, Pingu & Cassim - Mtu wa Watu

Artists: PNC, Z-ANTO, DOGO JANJA, PINGU & CASSIM MGANGA
Song: MTU WA WATU

NEW TRACK; SAJNA ft BELLE 9 & PIPI-ROHO MBAYA (PRODUCED BY DUKE)

Baada ya kipindi kirefu kupita msanii Faraji Twaha a.k.a Sajna ameamua kuachia wimbo wake unaoitwa 'ROHO MBAYA' ambao aliurekodi takribani miaka miwili iliyopita na kuwashirikisha Belle 9 pamoja na mwanadada Pipi.
Kwa mujibu wa Sajna wimbo huu sio official single yake ya mwaka huu lakini ameutoa kuvunja ukimya uliotokana na kubanwa na shule na pia kama zawadi kwa fans wake, wakati anajiandaa kutoa official song yake ya mwaka huu 2013. Roho mbaya pia inapatikana katika album yake ya kwanza inayoitwa Iveta.

Tuesday, January 15, 2013

NEW TRACK: MONSTAR - SIJAWASUSA (VUMILIA)

Artist: MONSTAR
Song: SIJAWASUSA (VUMILIA)
Studio: EXPENSIVE MUSIC
Producer: ZIDADAY MWAMBA

HUYU NDIO MWIZI ALIEIBA VITU KWENYE GARI LA MSANII MH TEMBA

Kwa mara ya kwanza juzi january 10 2013 ndio zilitangazwa habari za msanii Mh Temba kuibiwa vitu vya gari lake kwa mara ya tano, amekua na magari tofauti tofauti ambapo kwa mara tano ameibiwa vitu mbalimbali ambapo baadae amekua akilazimika kununua vitu vilevile vya kwake.
Hizi picha amezituma Exclusive kwa millardayo.com na kusema huyu jamaa anatuhumiwa kuwa mwizi hodari wa power window, vioo na vifaa vingine vya magari mbalimbali ambapo alipohojiwa na polisi amesema yeye huwa ananunua tu vifaa vya magari lakini hausiki kufanya wizi.

Wanaofanya wizi ni wengine ndio wanamletea na yeye anafanya kazi ya kumpigia simu mwenye mali ili aje avinunue vifaa vilivyoibiwa kwenye gari lake, sasa kilichofanya Mh Temba amkamate ni pale alipopigiwa simu na huyu huyu jamaa na kudai kwamba anavyo vifaa vilivyoibwa kwenye gari lake.
.

                                                 Hii ndio Verosa ambayo waliiba vifaa ambavyo baadae Temba alikuja kuvinunua kwa laki nane, na ni vifaa vilevile vilivyoibwa kwenye gari lake.
Kumbe huyu jamaa ndio yule yule aliwahi kumpigia simu Temba wakati alipoibiwa tena vifaa vya gari november 2012 na kumuuzia vifaa vilevile kwa shilingi laki nane huku Temba akiitoa hiyo pesa akiwa anajua kabisa vifaa anavyonunua ni vilevile, wakati huu Temba bado alikua ameisave namba yake kwa hiyo akashtukia mchezo kwamba jamaa ndio wanamchezea hivyo akajipanga na kwenda kumkamata.

Mtuhumiwa alipofikishwa polisi akajitetea kwamba yeye hausiki na wizi, yeye anafanya udalali wa kununua na kuuza hivyo vifaa tu na wala vitu vingine vinavyoibwa kwenye magari kama Camera na Laptop huwa hausiki navyo na wala havinunui.
Polisi wanamjua kabisa na namba yake wanayo kwa sababu jamaa amekua na kesi hizo mara nyingi sana hapo kituoni, mara ya mwisho ambapo wengi wanaoibiwa vifaa huwa anawaambia watume pesa kupitia line yake ya simu ya mkononi alafu wakishatuma ndio mtu anatumwa kwenda kuvipeleka hivyo vifaa, kama alivyofanya kwa Mh Temba mara ya mwisho na alitaka kufanya hivyo hata wakati huu.

Mh Temba amerudishiwa vifaa vyake alivyoibiwa wakati huu na mtuhumiwa ameachiwa, sio kwa dhamana ila wamechukua tu alama zake za vidole wakamwambia arudi jumatatu, Temba nae kaambiwa arudi jumatatu.

ALA KICHAPO BAADA YA KUNASWA AKILWAWITI WATOTO WADOGO:


Mwananchi huyu mwenye hasira kali akimnyanyua juu kibaka huyo na kumtupa chini kama akina 'John Cena'.
..Kichapo kikiendelea kwa kibaka huyo.
Kibaka huyo akizidi kuhukumiwa mtaani.
Ustadhi akijaribu kumnusuru kibaka huyo.
Ustadhi huyo aliamua kuondoka na kibaka ili kumwokoa.
Akimpeleka kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na eneo hilo la Shani.
KIJANA mmoja anayesadikiwa kuwa ni kibaka mchana huu amenusurika kifo baada ya kupokea kichapo kikali kutoka kwa wananachi wenye hasira wakimshutumu kuiba watoto wadogo na kwenda nao eneo la mto Morogoro chini ya daraja la Shani na kuwafanyia vitendo vya kihuni.
Akizungumza na Mtandao huu mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Juma Athuman alidai kwamba kijana huyo ana kawaida ya kuwateka watoto wadogo hasa wa shule na kuwapeleka chini ya daraja hilo na kuwafanyia vitendo vya kihuni.
" Kwa kipindi kirefu tulikuwa tukimsaka kibaka huyu ambaye ana tabia ya kuwateka watoto wadogo na kuwapeleka mto wa Morogoro chini ya daraja la Shani.
"Muda huu tumemfuma akiwa chini ya daraja hilo na mtoto mdogo ndipo tulipomfukuza na kufanikiwa kumkamata eneo hili la kituo cha mafuta jirani na daraja hili la Shani," alisema Juma Athuman.
Katika hatua nyingine 'ustadhi' mmoja alijitosa na kumnyakua kibaka huyo kutoka mikononi mwa kundi la wananchi hao na kumpeleka kituo kikuu cha polisi kilichopo jirani na eneo hilo la Shani SOURCE:
 

MATUKIO YA WANAFUNZI WA IFM WALIVYOCHEZEA KICHAPO KUTOKA KWA POLISI:



BAADA ya wanafunzi wa Chuo Cha Uongozi wa Fedha (IFM) kwenda kigamboni ambako Kamanda wa kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova kuwataka wakawasilishe hoja zao hukohuko ambako wanadai walipeleka majina ya wahalifu na hayajashughulikiwa, waligoma kufanya mkutano kwenye viwanja vya mpira eneo la Machava nakutaka mkutano huo ufanyike kwenye kituo cha polisi Cha Kigamboni ambako wanafunzi wengi wao walielekea huko.

VILIO NA KICHAPO TOKA KWA POLISI VILITAWALA MAANDAMANO YA YA WANAFUNZI WA IFM


Mwanafunzi aliyeshikwa akipandishwa kwenye Difenda.
Utakwenda Tu!


Mara baada ya kufika kwenye kituo hicho waliamriwa maratatu waondoke waende kwenye mkutano na Kamanda Kova wakakataa baada ya hapo ndipo mabomu yakaanza kupigwa. Kwenye mabomu hayo wanafunzi kadhaa walijeruhiwa na kuumia wengine walipoteza fahamu.

Hata hivyo walioshikiliwa wote waliachiwa na kutakiwa kwenda kwenye mkutano huo ambao uliazimia mambo kadhaa ya utekelezaji ili kutatua tatizo hilo la wizi kwenye eneo hilo. Kamanda Kova aliwaahidi wanafunzi hao kuwa watapata mrejesho wa hatua walizochukuwa siku ya tarehe 30 mwezi huu