Tuesday, January 1, 2013

HUYU NDIO DADA YAKE MARIO BALOTELLI AMBAE YUKO MAPENZINI NA MCHEZAJI OBAFEMI MARTIN.


.
Kwa wiki kadhaa sasa hivi zimekuwepo taarifa kwamba mchezaji wa Manchester City Mario Balotelli amekasirishwa na kitendo cha mchezaji wa Nigeria Obafemi Martins kuingia kwenye mapenzi mazito na dada yake, yani dada wa Balotelli.
Obafemi ameamua kuzungumza kwa kusisitiza kwamba hizo ni habari tu kwamba Mario kakasirika lakini sio kweli, Balotelli anafurahi dada yake kuwa mapenzini na Obafemi.

Wapenzi hawa wamekua wakionekana sehemu mbalimbali za goodtimes na wameonekana wazi kabisa kuwa kwenye mapenzi mazito.
Obafemi amekaririwa na Daily Post akisisitiza kwamba “Mario ni mshkaji wangu, ananiheshimu na mimi namuheshimu… habari za yeye kukasirika ni watu tu wanatunga”


Balotelli
Obafemi amesema ni kweli yuko kwenye mapenzi mazito na Abigail lakini hawana mpango wa kuoana sasa hivi na wala hawajawahi kuliongelea hilo.
Kwenye interview na gazeti la The Sun April 2012 Abigail ambae ni dada wa Mario Balotelli alisisitiza kwamba hana mpango wa kuwa mapenzini na mchezaji yeyote wa mpira kwa sababu ni watu wanaozungukwa sana na wasichana, wasichana wanajipeleka wenyewe bila kuitwa, hata Balotelli hatomruhusu kuwa na mpenzi mwanasoka lakini naona mambo yamekua tofauti sasa hiv

ASKARI ALIYEPIGA PICHA NA LEMA ATOROKA JESHINI


JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema askari anayedaiwa kuwa jeshi hilo aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ametoroka.
 
Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema jana kwamba pamoja na hatua yake ya kutoroka, jeshi litaendelea kumsaka kwa udi na uvumba ili kumhoji na kujiridhisha kama kweli ni mwanajeshi wake kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kifungu cha 147 cha Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya 1977.
 
“Huyu kijana inasemekana alishawahi kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), lakini wakati tunaendelea na uchunguzi alitoroka katika nyumba aliyokuwa amepanga bila ya taarifa kwa baba mwenye nyumba,” alisema Kanali Mgawe na kuongeza:
 
“Askari huyo alikuwa anaishi katika nyumba ya kupanga mita chache karibu na Kituo cha Polisi cha Simanjiro, Arusha na alikuwa akijishirikisha na ulinzi shirikishi.”
 
Alipoulizwa jina la askari huyo, Kanali Mgawe alijibu: “Yeye alikuwa anafahamika mtaani hapo kwa jina la kamanda.”
 
Hata hivyo, Kanali Mgawe alisema jeshi hilo litahakikisha linatoa ripoti kamili kwa umma baada ya kumkamata na uchunguzi kukamilika ili kuondoa utata uliogubika suala hilo.

Alipoulizwa kama kuna tofauti gani kati ya mwanajeshi kuingia kwenye mikutano ya wanasiasa na wale wanaofanya kazi za kisiasa kama wakuu wa wilaya na mikoa, Kanali Mgawe alijibu:” Wanajeshi wanaofanya kazi za U-DC au RC, wanaruhusiwa kisheria.”
 
Alifafanua kuwa iwapo mwanajeshi atateuliwa kufanya kazi katika taasisi yeyote ya Serikali nje ya jeshi, atatakiwa kuvua magwanda ya jeshi na kufanya kazi hiyo mpaka atakapomaliza muda wake na baada ya hapo ataruhusiwa kurejea jeshini.
 
“Kuna kitu kinaitwa ‘secondment.’ Mwanajeshi anaruhusiwa kufanya shughuli zozote nje ya jeshi iwapo atahitajika kufanya hivyo. Ila kwa masharti ya kuvua magwanda, hivyo wananchi wasishangae kuwaona baadhi ya askari wetu ni wakuu wa wilaya na mikoa na baadaye kurudi jeshini kuendelea na majukumu yao,” alisema Kanali Mgawe na kuongeza:
 
“Askari akiwa katika majukumu yake mapya, atafanya kazi zote atakazopewa zikiwamo za kisiasa kama ilivyo kwa wakuu wa wilaya na mikoa, lakini akirudi jeshini, anarudi kuwa askari mwenye utii na kufuata kanuni za jeshi zisizofungamana na siasa.”

RIPOTI FUPI YA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI- TANZANIA


Matokeo rasmi ya sensa yametoka. Idadi ya Watanzania ni milioni arobaini na nne nukta tisa. (44.9million).


Matokeo hayo yametangazwa leo katika viwanja vya Mnazimmoja jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.

Jumla: 44,929,002. TZ Bara 43,625,434 na Zanzibar 1,303,568
Source:MPEKUZI

MAJUU WAKISHANGILIA MWAKA MPYA WABONGO TUNASHEHEREAJE

 New Year's Eve celebrations around the world hapa Pakistan Rob Crilly... ukiwa mji umenuka mbaya kwa shagwe!!!


 Hapa watu wakiwa wanasherekeea kwa kuangalia  fireworks are lighting up the city's skyline



Australia welcomes in the New Year
• Revellers around the world prepare to celebrate the start of 2013
• India's army cancels New Year celebrations in remembrance of gang-rape victim
• Britain expects washout New Year as flooding countinues
• Record turnout expected for Hogmanay in Edinburgh

Tuesday, December 25, 2012

Weakening Xmas spirit should be re-energised


We are in the grip of yet another festive season, specifically Christmas that is due tomorrow, and which bears great significance to Christians, because it is the birthday of their saviour, Jesus Christ.
With the passage of time spanning over two thousand years, however, the significance of Jesus’ teachings, his crucifixion, death and resurrection has been progressively eroded. Jesus Christ, as son of God, is one of the constituents of the Holy Trinity – the others being the Father and the Holy Spirit – that highlights the baptism of Christians.
Christmas, therefore, should be a season of serious spiritual soul-searching and a chance for adherents to the faith to readjust themselves from sin to righteousness. The trend has been though, that, the season is characterised more by fanciful dressing, feasting, picnicking, and alcohol-indulgence sprees.
It is also an occasion for reunions of long-geographically separated relatives and friends; which is fine, only that, for most part, the re-unions represent crowds of merry-makers rather than seekers of positive spiritual revolution.
It is a trend that is worrying clerics and concerned worshippers, who are alarmed that, worldly life in which the quest for money, material possessions, and economic show-off, have been elevated to virtues, while the real virtues, such as leading simple lives, modesty, compassion and honesty, are being disregarded.
Worrying, too, is the proliferation of evangelical denominations whose focus is economic prosperity rather than advancement of Christian faith. But not all is well in mainstream churches, some of which are rocked by leadership wrangles, factionalism amongst worshippers, and the wayward tendencies of clerics and lay operatives in Church administrative establishments who should be role models but are bad example setters instead.
It is apparent, then, that, much clean-up has to be done, to whip stray Christian flock back onto the right path, for those whose faith has weakened to strengthen it, and, above all, for clerics to be paragons of spiritual virtue, since, after all, they are shepherds tasked to provide Jesus Christ-like guidance.
That will enrich the Christmas season. 
source:the Citizen

Wanawake marufuku kuvaa nguo fupi




Wanawake wa Swaziland
Wanawake nchini Swaziland wako katika hatari ya kukamatwa na polisi iwapo watavaa sketi fupi au blauzi ambazo zitaonyesha tumbo likiwa wazi.
Msemaji wa polisi Wendy Hleta amesema polisi watatekeleza sheria ya mwaka1889 ambayo inapiga marufuku uvaaji wa nguo zinazokosa maadili.
Msemaji huyo wa polisi pia amesema wanawake wanaovaa nguo fupi ni kivutio cha wabakaji.
Hata hivyo, sheria hiyo ya kikoloni haitumiki katika uvaaji wa nguo za kijadi ambazo zinavaliwa na wanawake, sehemu kubwa ya miili yao inaachwa wazi.
Mavazi hayo huvaliwa wakati wa sherehe, zikiwemo za mwaka zinazompa Mfalme fursa ya kuchagua mke wake mpya.
Mwaka 2000, serikali ilitunga sheria inayowataka wanafunzi wa kike kuanzia miaka 10 na zaidi kuvaa sketi zinazovuka magoti kama njia ya kuwalinda dhidi ya maambukizi ya Ukimwi.
Mfalme Mswati III wa Swaziland

Swaziland ina idadi ya watu milioni1.2 na moja kati ya nchi zenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya ukimwi duniani.


Bi Hleta amesema sheria hiyo ya mwaka1889 haijaweza kutekelezwa katika miaka ya karibuni.

Amesema polisi wanataka kuwajulisha wanawake kuwa sheria hiyo bado ipo na inafanya kazi.
Baadhi ya wanaume katika mji wa Manzini wamesemekana kuwalalamikia wanawake wanaovaa kuvaa nguo fupi.
source:BBC

Tuesday, December 18, 2012

PICHA ZA AJALI YA NDEGE YA TANAPA ILIYOTOKEA JUZI

Katongo ashinda tuzo ya mwaka ya BBC


Chris Katongo baada ya kupokea tuzo ya mwanasoka bora wa BBC
Christopher Katongo ameshinda tuzo ya mwanasoka bora wa BBC mwaka wa 2012.
Naodha huyo wa Zambia mwenye miaka 30 amemshinda Demba Ba, Didier Drogba, Younes Belhanda na Yahya Toure na kuwa mshindi wa kwanza kutoka Kusini mwa Afrika katika historia ya mashindano hayo.
Orodha ya washindani hao ilitengazwa na wataalamu wa soka Afrika, ambao wamezingatia umahiri wa mchezaji, uwezo wa kiufundi na ushirikiano na wachezaji wengine.
Na idadi kubwa ya watu wamepiga kura kupitia njia ya mtandao au ujumbe mfupi huku asilimia 40 kati yao wakimchagua Katongo, ambaye anachezea timu ya China Henan Construction.
 Katongo aandikisha rekodi mpya
Huku wachezaji wote walioorodheshwa katika kinyang'anyiro hicho walikuwa na mwaka mzuri, wanne kati yao walikuwa wameshinda medali mbali mbali, ni Katongo pekee ambaye mafanikio yake yamezingatiwa na mashabiki wa mpira Afrika.
Chris  Katongo
Chris Katongo akipokea tuzo hiyo kutoka kwa waziri
Katongo, ambaye ni mwanajeshi nchini mwake, alikuwa kivutio pindi alipoiongoza Zambia, katika michuano ya kombe la Mataifa Bingwa barani Afrika mnamo mwezi wa Februari mwaka huu.
Alifunga magoli matatu katika fainali iliyoandaliwa nchini Equatorial Guinea na Gabon na baadaye kufunga bao la ushindi kupitia mkwaju wa penalti na kuisadia Zambia kunyakuwa kombe hilo.
Zambia iliishindi Ivory Coast kwa 8-7 katika fainali hiyo baada ya timu hizo mbili kutoshana nguvu baada ya muda wa kawaida na muda wa ziada mjini Libreville.

Katongo afufua matumaini ya Zambia kuelekea Brazil


Chris Katongo akishika tuzo aliyoshinda
Kilikuwa ni kipindi kilichojawa na hisia kwa Zambia, ambayo miaka 19, iliyopita ilipata msiba mkubwa, pale ndege iliyokuwa imebeba wachezaji wa timu ya taifa ilipoanguka mita 500 tu mbali na Libreville, na kuuwa wachezaji wote 25 na rubani wake.
Miezi saba baada ya kuongoza Zambia kushinda kombe hilo, Katongo vile vile amekuwa nyota wa timu yake ya taifa wakati wa michuano ya kufuzu kwa fainali za mwaka ujao,wakati alifunga goli la pekee dhidi ya Uganda.
Bao hilo liliibuka kuwa bao muhimu sana kwa Zambia kwa kuwa ilipoteza mechi iliyofuatia kwa bao moja kwa bila, lakini ikafuzu kwa fainali za mwaka 2013 zitakazo andaliwa nchini Afrika Kusini baada ya kushinda kwa magoli 9-8 kupitia mikwaju ya penalti.

Mikakati ya kufuzu kwa kombe la Dunia

Na zaidi ya hayo yote, Katongo amechangua pakubwa harakati za kufufua matumaini ya Zambia ya kufuzu kwa michuano ya kombe la dunia ya mwaka wa 2014.
Chris  Katongo
Naodha wa Zambia Chris Katongo
Zambia ililazwa magoli 2-0 na Sudan mjini Khartoum mwezi Juni, matokeo ambayo hadi wakati huu hayajathibitishwa, huku uchunguzi ukiendelea kuhusu hatua ya Sudan ya kumshirikisha mchezaji ambaye hakuwa amesajiliwa.
Wiki moja baada ya mechi hiyo Zambia ilichuana na Ghana na Katongo kwa mara nyingine ndiye aliyefunga bao la ushindi na hivyo kuimarisha matumaini yao ya kufuzu.
Ikiwa Christopher Katongo ataendelea na hali aliyo nayo kwa sasa, huenda akaisaidia Zambia kuandikisha matokeo mazuri wakati wa michuano ya kuwania kombe la dunia nchini itakayoandaliwa nchini Brazil miezi kumi na minane ijayo.
Source:BBC

Monday, December 17, 2012

Dalili za "kuibiwa" penzi: How to know if your Girlfriend is cheating




Sometimes, a good relationship can be ruined by mistrusting your girlfriend. But there are always suspicions... How do you find out if your girlfriend is honest without putting your relationship at stake?

ADVISORY: The below are opinions based on personal experience from those who have experienced cheating on all ends. This is not a scientific method or anything sure-fire. Because this is relationship advice, it is infinitely complex, and requires serious finesse and strength of character.

Don't wait. If you have the feeling that your partner is cheating on you, it is best that you find out now rather than later. Having a thought of infidelity in your head can cause endless worry, leading to insecurities and doubt. Having these thoughts can destroy a relationship, real or imagined.


Observe. What led you to believe she may cheat? Is it her new "Friend"? Is she spending less time with you? Sharing less with you? Is she talking to or spending more time than usual with other men? Has she made any new single friends? Is she acting suspicious?

Watch for potential signs.

  • Does she send you text messages or calls less often? If you start being the one to call or text her first, that's a bad sign.
  • Secret phone conversations: Does your partner leave the room every time they get a call on their cell? Are they just trying to be polite? If your partner is trying to guard their conversations on the phone, there may be reasons to worry.
  • Distinct changes in appearances: If your partner suddenly starts worrying a little more about their appearance, (new cloths, always clean shaven, spending more time in the mirror) they may be trying to look good for someone else. If they get dressed up for you, that's one thing but if they seem to spend a little more time looking good to go out without you, you might want to look into that.
  • Picking fights: Is your partner picking fights and arguing more with you? This could just be an excuse to get out of the house. Picking a fight and then storming out of the house to get away from you is an easy way to go spend time with someone else.
  • Lying: Catching your partner in a lie no matter how small is always cause for concern. Try to connect lies with certain time frames and you may have a connection to infidelity.
  • Computer time: An increase in computer time may be one of the 7 signs you are being cheated on. There are many adult chat rooms out there that cater to infidelity. Check instant messaging, emails and so on.
  • Friends behavioral change: If your friends seem to feel uncomfortable around you, they may know something that you don't. A classic sign that your partner is cheating on you and you are the last to know.
  • Accusing you: Another common sign you are being cheated on is accusing you of the very same thing they are so guilty of, cheating. They may drop hints that you are having an affair because their own guilt is starting to wear on them.
Many women have no problems addressing concerns of infidelity as long as they are not accusations. If she becomes defensive or tries to turn the tables on you about your need to talk (i.e. making you feel horrible for asking), then it may be her guilt that is not allowing her to be honest with you about what's going on. This can often lead to a stalemate between lovers and cause havoc on even the tightest relationships.


Tell her you love her. Does she say it back? Hold her hand. Does she try to pull it away? Does she look nervous? These are signs that she might be thinking of cheating. However, some girls are shy and if the relationship is new, she may be uncomfortable with some things. Although, if it is new, she probably wouldn't be cheating, would she?


Many women in this day and age have confused sexualities because of shifting standards. Your girlfriend might be thinking of cheating on you if she is wanting to experiment either with kinks or other genders. Do not confront her about this. Instead, try looking for things in her web-browser history: Google searches, Wikipedia pages visited, maybe even porno sites. If you find anything like bondage, anal, or bisexuality, try bringing it up as if it were your fantasy. More than likely if she can find it at home, she won't go looking for it elsewhere.


Remember that the reason cheating is painful is not because of the act, but for all the reasons it took place. Do not focus on the cheating act - try and repair or confront any relationship troubles. Either your relationship will end or it will be better than before, and either way, the majority of the time, she will confess to cheating or to considering it.


Ask her friends (not "IS she having an affair"), but about her regular activities. Then, you will be able to get some tips. Unfortunately, you are usually the last to know that she's thinking of cheating. Look for changes in her friends behavior. Are they hanging out with you less as a couple? Most people unconsciously act differently towards those they know are being deceived. Although they may sympathize with your situation, they are unlikely to rat out a friend.


Ask her about her opinion on a specific guy. If she hesitates to answer or becomes defensive or inconsistent, then chances are you might want to have a closer look at that specific relationship.


Like the old saying goes, "Once a cheater, always a cheater". Has she snuck around other boyfriends in the past? If so, then, she is 2.5 times more likely to cheat then those who have never before. Tread carefully with these women.

In the end, follow your gut instinct. Sometimes, you just know things without having to second-guess yourself. No amount of crying and denial can rival the feelings you have in the pit of your stomach. After you've taken all the evidence into consideration, it's time to follow your gut. If she's thinking of cheating or has a wandering eye, chances are she thinks she can do better. If so, then maybe you can too.


If you find out she's cheating, discuss it with her. If she cheated out of ignorance or sexual confusion and genuinely regrets it, you should consider forgiving her. If she doesn't seem to care, dump her and find someone who appreciates you.


Remember it's not your fault. There are a myriad of reasons to break up with someone but only one reason to cheat. It is a personal failing on the cheater, not the cheated. Because if you didn't complete them, then they should break up with you; not cheat on you. So even if you are the worst person in the world, the only reason to cheat is because they have a problem, not you.

Source: Mtandao

Dk. Bilal awaasa Waislamu kuepuka vurugu

MAKAMU wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, amewataka Waislamu nchini kufuata kanuni za msingi za Kiislamu, ili kuepuka vurugu, machafuko na uharibifu wa mali kama zilizotokea hivi karibuni.
Dk. Bilal alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, wakati wa hafla ya kuupokea Mwaka Mpya wa Kiislamu (1434), Hijiriya, iliyoandaliwa na Jumuiya ya Kiislamu ya Istiqama. Alisema utaratibu huo wa Kiislamu ni muhimu, hivyo unapoachwa kufuatwa huweza kusababisha machafuko na kuuana kwa kisingizio cha dini.
Dk. Bilal alisema kanuni za msingi wa Kiislamu ndizo zinazolinda dini hiyo na Waislamu wenyewe pamoja na dunia nzima, huku kanuni hizo zikiwa chanzo cha kujipima na ndizo zinazofanya Uislamu kuitwa Uislamu.
Alisema Uislamu na Waislamu hawana budi kufuata kanuni za msingi, ili wausaidie Uislamu na nchi yao ambapo njia ya msingi ni elimu.
“Kwa mawazo yangu matatizo mengi yanayolenga Uislamu ni ukosefu wa elimu, elimu ya Uislamu wenyewe na elimu nyingine ya dunia,” alisema Dk. Bilal.
Aliongeza kuwa aya za mwanzo alizoshushiwa Mtume Muhammad (SAW), ni kusoma, hakuambiwa kusali au kufunga bali alitakiwa kusoma.
Naye Mwanazuoni Profesa Usamah Ismail Mohamed, aliwausia Waislamu kuwa na tabia njema ambayo inaweza kuwasaidia kufanya wengine wasio Waislamu kuhamia katika dini hiyo.
Kwa upande wake, Sheikh wa Jumuiya hiyo, Juma Nassoro Alhina ameiomba serikali kuifanya siku hiyo kuwa ya mapunziko kila inapofika kama ilivyo katika sikukuu ya miezi ya kawaida (Januari hadi Desemba). 
Source:Tanzania Daima

JK aandaliwa M4C

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), imemaliza kikao chake cha siku mbili jijini Dar es Salaam, na kuazimia kuanza Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) kwa ajili ya kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete, atekeleze madai yao.
Katika kikao hicho, mbali na ajenda nyingine, wajumbe walipokea na kujadili taarifa ya utekelezaji kutokana na maazimio ya kikao cha dharura kilichokutana Septemba 9, mwaka huu.
Miongoni mwa maazimio hayo, ilikuwa na kupata majibu ya utekelezaji wa madai yao katika barua rasmi waliyomwandikia Rais Kikwete kupitia kwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.
Baadhi ya masuala hayo ambayo yaliazimiwa ni kuwataka Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema, Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile wawajibike kwa kujiuzulu nafasi zao au wafukuzwe kazi.
Kwamba kwa kuzingatia kuwa, mauaji kadhaa yalitokea mikononi mwa Jeshi la Polisi, vile vile waliazimia kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda, Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Morogoro na askari waliosababisha mauaji ya raia wasio na hatia Morogoro na Iringa wafikishwe mahakamani kujibu mashtaka ya mauaji.
Chanzo chetu cha siri kutoka ndani ya kikao hicho, kilieleza kuwa wajumbe walielezwa kuwa rais amesema kuwa ataifanyia kazi barua hiyo, na hivyo CHADEMA katika kutilia mkazo, waliazimia kufanya operesheni hiyo kama shinikizo.
“Kwa hiyo kuanzia Januari mwakani, M4C itaanza rasmi ili kumshinikiza Rais Kikwete atekeleze matakwa ya barua yetu kwa kuwaondoa viongozi hao waliosababisha vifo vya raia wasio na hatia.
Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hivi karibuni waliwaonya viongozi wa chama chake kuacha kutegemea nguvu ya Jeshi la Polisi katika kukabiliana na hoja za wapinzani.
Alisema kuwa, hoja za kisiasa zinajibiwa kisiasa, lakini akaeleza kushangazwa na hatua ya viongozi wa CCM kukimbilia kuomba nguvu ya polisi wakati wapinzani wanapoibua tuhuma dhidi ya chama hicho.
Kikao hicho cha siku mbili, mbali na kupokea taarifa hiyo kuhusu Rais Kikwete, pia kilijadili ajenda tatu ambao ni taarifa ya hali ya siasa nchini, mchakato wa mabadiliko ya katiba ya nchi na operesheni ya M4C.
Viongozi wakuu wa CHADEMA wamekuwa wakimkumbusha Rais Kikwete kujibu barua yao na kuwachukulia hatua wahusika ili kuondoa hofu ambayo imetawala kwa umma kuhusu mauaji ya raia yanayozidi kujitokeza.
Katika barua hiyo kwa Rais Kikwete, walitoa wito wakimtaka aunde tume huru ya kiuchunguzi ya kimahakama (Judiciary Commission of Inquiry) kuchunguza vifo vilivyotokea katika mazingira tata katika mikoa ya Arusha, Tabora, Singida, Morogoro na Iringa.
Source:Tanzania Daima

KWA WALE WANOPENDA MAGARI,PICHA KUMI YA MAGARI MAKALI:










Friday, December 14, 2012

Wafufua maiti na kuitembeza mitaani

NewsImages/6711370.jpg Mmoja ya maiti ikipambwa kabla ya kufanyiwa sherehe
Wakazi wa Jimbo la Twaraj Indonesia, wamejiweka utamaduni wa kuwafufua maiti(wafu) na kuwapamba kwa kuwavisha mavazi mapya, kuwachana nywele na kuwatembeza mitaani kabla ya kuwazika tena
Dunia imejaa vituko na matukio ya ajabu, hilo limedhihirika hivi karibuni huko nchini Indonesia, katika jimbo la Twaraj, wakazi wa eneo hilo wanatamaduni ya ajabu na ngeni duniani, wakazi hao wanawafufuwa maiti kaburini na kuwavalisha nguo mapya za thamani, kuwachana nywele na kuwapamba kamalive walivyokua hai.

Wakazi hao wanakusanyika na kumfanyia sherehe kubwa maiti kabla ya kuanza msafara wa kumtebeza katika mitaa na kumrejesha kaburini alipokuwa amezikwa, wakazi hao wanamini kwamba watu waliyokufa wanahaki ya kuendelea kuishi na kujumuika nao.

katika kufanikisha zoezi hilo la kihistoria ambalo wanaimani kwa lazima kufanya ili kuonesha hishima kwa maiti na kulinda mapenzi ya kweli kwa mtu aliyekufa, kabla ya kumzika maiti anavishwa kitambaa maalum ili kuzuia mwili wa marehemu kuoza.

Mnyika: Vyombo vya uamuzi viwe huru

na Farida Ramadhani

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), ametaka Katiba ijayo ivipe mamlaka kamili vyombo vya uamuzi kwa lengo la kuviwezesha kufanya kazi kwa uhuru pasipo kuingiliwa na mamlaka zingine.
Mnyika alitoa maoni hayo jana wakati akichangia mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya katika mkutano uliofanyika kwenye kata ya Makurumla, jijini Dar es Salaam.
Mbali ya kutaka uhuru kwa baadhi ya taasisi, pia Mnyika alitaka Katiba mpya ieleze wazi kuhusu haki ya kupata elimu, kumiliki uchumi wa nchi kwa wananchi na upatikianaji wa maji ya uhakika ni haki inayoweza kudaiwa mahakamani.
Alisema Katiba ijayo iwawezeshe wananchi kuwatimua viongozi wa ngazi ya udiwani na ubunge ikiwa wataenda kinyume na matarajio ya uwepo wao madarakani.
Alivitaja vyombo ambavyo vinapaswa kuwa huru kuwa ni pamoja Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ofisi ya Mwendesha Mashataka (DPP) na maeneo mengine ya uamuzi kama Bunge akisema kwa sasa havina uhuru wa kutosha wa kufanya kazi pasipo kuingiliwa na muhimili mwingine.
“Leo hii wabunge tukijidai kukataa bajeti ya serikali, Rais anaweza kulivunja Bunge na yeye akabakia na urais wake; hili suala lazima liangaliwe kwa umakini katika Katiba ijayo. Tusitoe nafasi ya kumfanya mtu mmoja kuwa na nguvu zilizopitiliza,” alisema Mnyika.
Alisema kwa taasisi kama TAKUKURU, DPP na zingine za Kikatiba ni lazima wanaopata fursa ya kufanya kazi waingie kwa sifa za kuomba badala ya kuteuliwa na Rais hali inayowafanya wasiwe na uwezo wa kuhoji sehemu yenye kuhisiwa kuwa na maslahi na uongozi wa juu wa nchi.
Katika kudhibiti ufisadi na kuongeza uwajibikaji, Mnyika alitaka Katiba mpya ihimize upendo na uwe msingi mkuu wa uwajibikaji kwa kila anayepata fursa ya kuwatumikia wananchi katika ngazi yoyote.
Katika utoaji wa maoni hayo Mnyika alionyesha wasiwasi wake wa kupatikana Katiba ya wananchi kwa kile alichoeleza kuwa watakaopitia maoni ya wananchi ni tume ileile iliyoteuliwa na mtu mmoja.
Alitaka tume ya sasa ya kukusanya maoni iandae ripoti ya mapendekezo na marekebisho maalumu na kuwa kuwe na tume huru itakayosimamia maoni ya wananchi yanayokusanywa.
Katika utoaji huo wa maoni, baadhi ya wananchi walitaka nafasi ya wakuu wa wilaya na mikoa kama kuna haja ya kuwepo ziwe ni za kupigiwa kura tofauti na zilivyo sasa ambapo wahusika huteuliwa.
Mapema asubuhi, tume hiyo ilikusanya maoni kwa wakazi wa Makuburi na Mabibo ambapo walipendekeza kuwa Katiba mpya izuie uwepo wa shule na hospitali za watu binafsi.
Mbele ya mjumbe wa tume hiyo, Ester Mkwizu, mwananchi mmoja Abbas Benard alisema kuwa uwepo wa shule na hospitali za watu binafsi unaongeza matabaka katika jamii na kuzidi kukandamiza watu wa hali ya chini.
Alisema kuwa viongozi na familia zao wanatibiwa kwenye hospitali binafsi na kuacha hospitali za serikali zikiwa hazina dawa, kitu ambacho kiko hata kwenye elimu.
“Shule za serikali hazina walimu na hazina vitabu, kwa hali hii mtoto wa maskini atajikomboa kweli?” alihoji Benard.
Alipendekeza mahakama kumchagua Jaji Mkuu badala ya kuteuliwa na Rais ambaye anateuwa viongozi wengi kulingana na mamlaka aliyokuwa nayo.
Naye Masoud Kaftany, alisema kuwa Katiba ya sasa iendelee kutumika, lakini baadhi ya vitu inabidi viongezwe na vingine vipunguzwe.
Kaftany alisema kuwa anapendekeza umri wa kugombea urais uwe kuanzia miaka 40 hadi 65 wakati umri wa kugombea ubunge uwe kuanzia miaka 21 hadi 55, tofauti na ilivyokuwa katika Katiba ya zamani.
Alipendekeza kutolewa kwa viti maalumu vya wabunge na kupunguzwa kwa vyama vingi, vibakie vitatu ili kuzuia matumizi makubwa ya ruzuku ya serikali katika vyama hivyo.
Naye Harieth Raphael, alipendekeza kuwe na marekebisho ya sheria kandamizi hasa dhidi ya mwanamke na mtoto wa kike kama sheria ya umiliki wa aridhi na haki za mirathi.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Daniel Kimaro, ambaye alisema kuwa Katiba mpya isimuangalie mwanamke pekee kwani hata wanaume pia wananyanyasika kijinsia.

KUNA TOFAUTI GANI KATI YA HIZI PICHA 2 INGAWA WOTE WANAJENGA?



NI KWELI HUU NI MWISHO WA MR.BEAN?



LONDON, ENGLAND
ANAWEZA kuwa mchekeshaji maarufu zaidi duniani kwa kipindi cha miaka 20 iliyopita, lakini kwa sasa kuna kila dalili kwamba huenda siku za kuigiza za Rowan Atkinson Mr Bean zikawa zimefika mwisho baada ya kuonyesha kuchoshwa na kazi hiyo.

Mashabiki wa Mr. Bean wanaweza kuanza kumtafuta mtu mwingine wa kuwachekesha baada ya mwigizaji huyo kutoa ishara kuwa anastaafu katika kazi hiyo iliyompatia umaarufu mkubwa na utajiri wa kutosha.
Kazi hii imekuwa ya mafanikio makubwa ya kibiashara kwangu, hata hivyo kimsingi imekuwa ngumu na inazidi kuwa ya kitoto. Hata hivyo najisikia kuendelea kuifanya kidogo zaidi, alisema akiliambia gazeti la Daily Telegraph.

Achilia mbali ukweli kwamba uwezo wa nguvu unapungua, lakini nadhani pia inahuzunisha wakati mtu unapokuwa na miaka 50 halafu inabidi uonekane kama mtoto.
Mr. Bean, ambaye sasa ana umri wa miaka 57 anasema anajisikia kuendelea kucheza filamu ambazo zitamfanya aonekane kuwa mtu makini zaidi huku akikiri kwamba filamu za ujinga alizocheza huenda zikaathiri watazamaji ambao wanamuona zaidi kama mchekeshaji kuliko mtu makini.

Jina la Mr. Bean lilipata umaarufu zaidi ya jina lake la Atkinson wakati akisoma masomo yake ya Shahada ya Uzamili (Masters) katika Chuo Kikuu cha Oxford. Kuanzia hapo aliachia tamthiliya zake zilizompatia umaarufu duniani kote kuanzia mwaka 1990-1995.

Mr. Bean alionekana kuwa na kipaji kikubwa cha kuonekana kama mtoto katika umbo la mtu mzima huku akimudu kwa ustadi mkubwa vipingamizi mbalimbali ambavyo vilimkabili katika maisha yake ya kila siku.

Mara zote alifanya kila kitu kwa umakini mkubwa bila ya kuongea neno lolote na kuwafanya watazamaji wacheke zaidi huku yeye mwenyewe akiwa kimya kama ilivyokuwa kwa mchezeshaji maarufu wa zamani, Charlie Chaplin.

Blair, Wenger wafananishwa naye
Kutokana kwa umaarufu wa tabia zake za kitoto na kijinga, watu wengi maarufu wamekuwa wakifananishwa naye pindi wanapochemka katika masuala mbalimbali yanayowahusu.
Jina Mr. Bean huchukuliwa sawa na tusi kwa wale wote wanaoonekana kichekesho mbele ya jamii.

Katuni maarufu ya Homer Simpson iliwahi kumkejeli Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair ikimlinganisha na Mr. Bean kutokana na kile kilichoonekana kuburuzwa na utawala wa Marekani uliokuwa chini ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, George Bush.

Waziri Mkuu wa zamani wa Hispania, Jose Luis Rodriguez Zapatero aliwahi kuandamwa na raia wa nchi yake waliokuwa wanamfananisha na Mr. Bean kutokana na namna alivyoonekana kuendesha mambo ovyo ovyo katika serikali yake.

Kocha maarufu wa Arsenal, Arsene Wenger, ambaye kwa sura anafanana kiasi na Mr. Bean, pia amekuwa akifananishwa na msanii huyo na baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo kutokana na kuonekana kuishiwa mbinu za kuiendesha timu iliyoshindwa kutwaa taji lolote kwa kipindi cha miaka saba sasa.

Ana utajiri wa kutisha
Mpaka sasa, Mr. Bean ndiye staa wa televisheni mwenye utajiri mkubwa zaidi Uingereza, shukrani kwa umaarufu wake alioupata kwa uchekeshaji huo ingawa pia amekuwa akicheza filamu nyingine.

Mr. Bean ana majumba ya kifahari katika miji ya Chelsea na Oxford, huku pia akiwa anaendesha magari ya kifahari hasa yale ya mwendo wa kasi.

Anamiliki magari aina ya Honda NSX, Audi A8, Honda Civic Hybrid, Renault 5 GT Turbo, McLaren F1 na mengineyo.
Kwa ujumla anakadiriwa kuwa na utajiri unaofikia Pauni 100 milioni (Sh 252.5 bilioni). Mpinzani wake wa karibu anatajwa kuwa mwandaaji wa vipindi vya Who Wants To Be A Millionaire, Chris Tarrant, ambaye anatajwa kuwa na utajiri unaofikia Pauni 50 milioni (Sh126.2 bilioni).

Filamu alizocheza kama Mr. Bean pekee zimempatia kiasi cha Pauni 11 milioni (Sh 27.7 bilioni) huku zikiwa zimeuzwa katika nchi 94 duniani kote. Kiasi kingine cha pesa amejikusanyia katika matangazo mbalimbali ya biashara na kampuni kubwa.

Familia yake
Mr. Bean ni mtoto wa mwisho katika familia ya watoto wanne, wote wa kiume. Alizaliwa huko Consett, County Durham, England Januari 6, 1955 na baba yake ni Eric Atkinson ambaye ni mkulima. Mama yake ni Ella May. Kaka zake ni Paul (marehemu), Rodney na Rupert.
Ana mke aitwaye Sunetra Sastry aliyekuwa anafanya kazi BBC na walioana Februari 5, 1990 katika Jiji la New York, Marekani.

Wana watoto wawili na wanaishi Apethorpe, Northamptonshire ambapo pia ni karibu na uwanja wa zamani wa Arsenal, Highbury jijini London.
Kabla ya ndoa yake, Mr. Bean aliwawahi kuwa na uhusiano wa karibu na mwigizaji maarufu wa filamu, Leslie Ash.

‘Tunamsubiri Dk Ulimboka atoe taarifa’

Kwa ufupi
“Sijanunuliwa, sijawaogopa watesi wangu, wala sijanyamazishwa kwa lolote lile. Hata hao wanaoeneza taarifa kuwa nimenunuliwa, wanajua kuwa hawana ubavu wa kuninunua. Bali kimya changu kimetokana na kufuata masharti ya daktari wangu,” ameeleza Dk Ulimboka kujibu swali iwapo kimya chake kimetokana na kununuliwa.
Mwenyekiti wa Madaktari Tanzania,Steven Ulimboka 
JESHI la Polisi nchini limeibuka na kusema linamsubiri Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka kufika polisi na kutoa taarifa yake rasmi kuhusu tukio lililomtokea Juni 26, mwaka huu.
Akizungumza na Mwananchi jana, msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso alisema kuwa, wanamsubiri Dk Ulimboka afike polisi na kutoa taarifa yake rasmi pamoja na ushirikiano ili wapate kujua nini kilichotokea.
“Wakati ule hatukumhoji kwa kuwa alikuwa anaumwa tokea hapo, hatujapata taarifa yake hivyo, sisi tunamsubiri aje kutoa taarifa yake na atupe ushirikiano katika suala hilo,” alisema Senso na kuongeza:
“Tunataka kujua hali yake, lakini sisi tunamsubiri aje ili tupate ushirikiano wake.”
Kabla ya polisi kutoa taarifa hiyo jana, Oktoba 28, mwaka huu, Dk Ulimboka aliibuka na kusema yuko imara na anajiaanda kuanika waliomteka, kumtesa na kisha kumtupa katika Msitu wa Mabwepande, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Dk Ulimboka alisema kuwa kamwe hajanunuliwa na kuwa kwake kimya kwa muda mrefu kumetokana na kufuatilia kwa karibu masharti ya matibabu yake na si vinginevyo.
“Sijanunuliwa, sijawaogopa watesi wangu, wala sijanyamazishwa kwa lolote lile. Hata hao wanaoeneza taarifa kuwa nimenunuliwa, wanajua kuwa hawana ubavu wa kuninunua. Bali kimya changu kimetokana na kufuata masharti ya daktari wangu,” ameeleza Dk Ulimboka kujibu swali iwapo kimya chake kimetokana na kununuliwa.
Dk Ulimboka alikiri kuwa amewahi kusikia taarifa za yeye kununuliwa na kwamba huwa anajisikia vibaya anapoona kuna kundi la watu linahaha kutaka kupotosha ukweli na kuchafua jina lake.  
“Huo ni uzushi mtupu. Hata walionitesa wanajua kuwa hawawezi kuninyamazisha au kuninunua. Wanajua sina bei katika kutetea masilahi ya Umma. Ndiyo maana wakaamua kutumia njia ile ya kinyama kutaka kunitoa roho yangu. Siwaogopi wanaodhuru mwili bali yule awezaye kutoa roho. Nakuhakikishia, muda si mrefu nitaanika kila kitu juu ya kutekwa kwangu, kuteswa na kutupwa kwenye msitu wa Mabwepande,” ameeleza.
Juni 26, 2012, Dk Ulimboka alitekwa kuteswa kusukumizwa kwenye gari, kupigwa, kufungwa mikono na miguu, kunyofolewa kucha na kutolewa meno na hatimaye kutupwa katika msitu wa Mabwepande.
Mwenyekiti huyo wa Jumuia ya Madaktari Tanzania , aliokolewa asubuhi yake na wasamaria wema karibu na msitu huo, Bunju nje kidogo ya Dar es Salaam.
Akizungumza kwa sauti ya kujiamini, Dk Ulimboka, ambaye bado hajahojiwa na polisi wa Tanzania juu ya aliowataja, amesisitiza kuwa alipokamatwa alikuwa na akili timamu na kwamba waliopanga mkakati wa kumteka anawafahamu.
CHANZO:GAZETI LA MWANANCHI

WACHEZAJI WA ZANZIBAR WAPIGWA MARUFUKU



Timu ya soka ya Zanzibar
Timu ya soka ya Zanzibar
Shirikisho la mchezo wa Soka visiwani Zanzibar,ZFA limechukua uamuzi ambao umewashngaza sana mashabiki wengi wa soka, visiwani humo, nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.
Kwa mujibu wa ripoti maafisa wakuu wa ZFA wamewapiga marufuku wachezaji wake wote walioshiriki katika michuano ya kuwania kombe CECAFA Senior Challenge, iliyokamilika nchini Uganda, kutoshiriki katika mechi yoyote popote duniani kwa muda usiojulikana.
Aidha ZFA limeamua kuvunja timu ya taifa maarufu kama Zanzibar Heroes, licha ya kuwa timu hiyo ilimaliza katika nafasi ya tatu katika michuano hiyo ya CECAFA.
Baadhi ya wachezaji hao waliopigwa marufuku ni pamoja na nyota na naodha wa Yanga, Nadir Haroub.

Kwa nini ZFA ilichukua hatua hiyo?

Nadir Haroub
Nadir Haroub naodha wa Yanga
Wachezaji hao wanakabiliwa na tuhuma za utovu wa nidhamu.
Akitoa tangazo hilo, katika makao makuu ya shirikisho hilo, makamu wa rais wa ZFA Alhaj Haji Ameir, alisema wanachama wote wa kamati kuu ya ZFA kwa kauli moja waliafikiana kuhusu hatua hiyo, ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine.
Kamati hiyo ya ZFA iliitisha kikao cha dharura, baada ya wachezaji hao wa Zanzibar Heroes, kugawana fedha walizoshinda wakati wa michuano hiyo ya CECAFA.
Zanzibar ilimaliza katika nafasi ya tatu na hivyo kujishinda dola elfu Kumi za Kimarekani.
Ripoti zinasema fedha hizo ziligawanywa na wachezaji hao kama njia moja ya kuwasilisha malalamishi yao kwa ZFA kuhusiana na jinsi wao wanavyoshughulikiwa wakiwa kambini.
Inadaiwa kuwa wachezaji hao waliamua kugawana fedha hizo kwa madai kuwa wamekuwa wakidhulumiwa fedha zao na ZFA.
Baadhi yao wanasema ZFA huwa na mazoea ya kuchukua hela zote wanazoshinda bila hata kuwapa chochote ili hali wao ndio waliofanya kazi zaidi.

Kinyume na matarajio ya wengi kocha mkuu wa Zanzibar Heroes, Salum Bausi ambaye kujiuzulu baada ya mashindano hayo ya CECAFA, amewashangaza wengi kwa kuunga mkono, uamuzi huo akisema wachezaji hao wameharibu sifa ya Zanzibar.
Hata hivyo kuna baadhi ya wachezaji walioamua kurejesha fedha walizopewa kwa shirikisho hilo na ZFA haijatoa orodha yao.
CHANZO:BBC

HUU NDO UKWELI KUHUSU UVUMI WA MIKE TYSON KUJIBADILI JINSIA

Vyombo vya habari nchini hususan magazeti leo vimeamka na vichwa vya habari kuhusiana na taarifa iliyoenea mtandaoni kuwa bingwa wa zamani wa ndondi duniani Mike Tyson amefanyiwa upasuaji na kubadilisha jinsia yake kuwa mwanamke.
Magazeti yalioandika habari hiyo ni pamoja na Mwananchi ‘Tyson adaiwa kubadili jinsi’, gazeti la Jambo Leo ‘Tyson awa Mwanamke’ na vyombo vingine.


 Kwa kujiamini tunasema magazeti hayo yameingia ‘chaka mbaya’. Habari hiyo imeandikwa na mtandao wa http://www.newsbiscuit.com/ ambao asilimia 100 ya habari zake ni za kutunga.
Habari hiyo inasema Mike Tyson sasa ataitwa Michelle baada ya kufanyiwa upasuaji katika hospitali moja ya huko Beverley Hills nchini Marekani . Habari hii imeripotiwa na mitandao tofauti tofauti, pia gazeti la The Standard.
Habari hiyo inasema vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu akisema itakuwa amekamilisha ndoto yake pale atakapoanza kuona siku zake (hedhi), na kusema kuwa ili kukamilisha dhamira yake ya kuwa mwanamke’ jina lake ataitwa Michelle.
Kuna mambo mengi yanayoifanya habari hii iwe na walakini na kutufanya moja kwa moja tuamini kuwa si ya kweli. Kwa asilimia nyingi hii ni ‘hoax’ (a deliberately fabricated falsehood made to masquerade as truth.) Yaani ni habari ya ya uongo ama iliyotengenezwa ili kuifanya ionekane kama ya kweli.
Hizi ni sababu kubwa za kwanii hii ni habari ya uongo:

1. Habari hii inaonekana kutoka kwenye chanzo kimoja (newsbiscuits) na vyombo vingine vimekuwa vikiichukua kama ilivyo, neno kwa neno. Habari yenyewe ni hii:
America — Former undisputed heavyweight boxing champion of the world Mike Tyson is said to be “feeling fine” after undergoing successful gender reassignment surgery at a clinic near Beverley Hills.
Once known as “The Baddest Man on the Planet”, the boxer said having his first menstrual cycle “would be a dream come true”, and that from now on he would be known as Michelle.
“Some people might think it strange that I’m now a woman,” said Tyson, who underwent complete facial feminisation, orbital bone contouring and nasal surgery in an operation lasting over 16 hours.
‘But even at the height of my career, when pound for pound I was regarded as the best fighter in the world, I never lost touch with my feminine side and knew that one day I would grow breasts and have a vagina.’
Iron Mike was given the all-clear for gender reassignment surgery following a successful course in hormone replacement therapy which, in his autobiography, the boxer blamed for his 1996 defeat at the hands of Evander Holyfield.
Although at the time Tyson insisted he was fit enough to carry on with the fight, referee Mitch Halpern stopped the bout in the 11th round saying Tyson looked flushed, was sweating profusely and appeared to be lactating heavily from his left breast.
Tyson, said he hoped being female would finally convince the American people that his “bad-boy” days were over and he had turned over a new leaf.
2. Vyombo vinavyoheshimika kwa kuandika udaku duniani havijaandika habari hii.Kama ingekuwa kweli, hii ni habari kubwa mno kuachwa kuandikwa na mitandao kama The Sun, TMZ, mediatakeout na mingine. Hii ingekuwa habari kubwa mno pengine kuzidi hata kesi ya kulawiti watoto iliyokuwa ikimkabili Michael Jackson.
Jaribu kugoogle jina Mike Tyson kwenye sehemu ya ‘news’ na uone ni vyombo gani vimeandika habari hii. Umaarufu wa Mike Tyson duniani ungeifanya habari hii kutoandikwa na vyombo vya habari vya udaku tu bali pia mashirika makubwa kama BBC, CNN, Al-Jazeera na mengine yangetengeneza makala ndefu zenye undani mkubwa wa habari hii.
3. Akaunti zake mitandao ya kijamii hazioneshi mashabiki wake kuichukulia maanani habari hii. Tunafahamu jinsi mitandao ya kijamii inavyowaunganisha mastaa na mashabiki wao. Nenda kwenye akaunti ya Twitter ya Mike Tyson na angalia kama kuna mashabiki wanaomuuliza Tyson juu ya ukweli wa habari hii, Hakuna. Sababu ni kuwa hakuna kitu kama hicho na wengi wao hawana muda wa kuifuatilia.
4. Mike hawezi kuchukua uamuzi wa fedheha kama huo. Mike ni kitambulisho cha ujasiri na uanaume wa shoka, sio rahisi kujigeuza kuwa mwanamke, I mean come on Tyson anaweza kujigeuza kuwa mwanamke kweli?
Kwa asilimia 100 hii ni habari ya kutunga na ya uongo kama zile habari za wasanii kudaiwa kufa kwenye ajali. Bila utafiti hakuna haki ya kuongea.
Habari zingine za uongo zilizoandikwa na mtandao huo ni pamoja na ‘Abramovich amtaja Abramovich kuwa kocha wa Chelsea’, ‘Ndoa ya kwanza ya jinsia moja ya Nick Clegg na David Cameron yafungwa’, ‘Hatimaye Mungu akubali kumsaidia Malkia’, ‘Mgogoro wa mashariki ya kati wasuluhishwa kwenye Twitter’ na zingine nyingi.

CHANZO:Bongo 5

KADHI MKUU AMKANA PONDA

Kwa ufupi
Baada ya kuambiwa hivyo, Habibu alidai kuwa hakuna hata mmoja anayefamfahamu katika utendaji wa kazi za Uislamu kama kiongozi kwenye baraza lakini akawatambua kimavazi kuwa ni waumini wa Kiislamu. “Ila kwa kuona, muungwana ishalaa inamuonyesha kuwa kuna baibui, kanzu na kofia (baraghashia) inaonekana kuna Waislamu na wasio Waislamu.

  Shekhe Ponda Issa Ponda

KADHI Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Habibu (49) amekana kumfahamu Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Shekhe Ponda Issa Ponda na wafuasi wake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Habibu alikana kumfahamu Ponda na wafuasi wake jana Mbele ya Hakimu Mkazi, Ritha Tarimo mara baada ya kutakiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka awatazame kina Ponda na aelezee iwapo kuna mmoja aliwahi kuingia kwenye Baraza la Maulamaa wa Bakwata.

Baada ya kuambiwa hivyo, Habibu alidai kuwa hakuna hata mmoja anayefamfahamu katika utendaji wa kazi za Uislamu kama kiongozi kwenye baraza lakini akawatambua kimavazi kuwa ni waumini wa Kiislamu. “Ila kwa kuona, muungwana ishalaa inamuonyesha kuwa kuna baibui, kanzu na kofia (baraghashia) inaonekana kuna Waislamu na wasio Waislamu.”

Akiendelea kutoa ushahidi wake, Kadhi huyo aliiambia mahakama ; “Nathibitisha kuwa Kampuni ya Agritanza Ltd inamiliki lile eneo kwa Uhalali na kwamba haikupita uchochoroni ikaruka ukuta ikaingia ndani ya hilo eneo, ilifuata utaratibu na kupokea hati zote na haki yake,” alisema Habibu.

Alifafanua kuwa Baraza la Maulamaa ni chombo kinachotoa uamuzi ya mwisho na kutoa miongozo mbalimbali kwa Waislamu na kwamba Bakwata inawakilisha Waislamu wote Tanzania.

Alidai kuwa Baraza hilo la Maulamaa linaundwa na wajumbe 10 kutoka mikoa mbalimbali na kwamba mjumbe huteuliwa kutokana na kuwa na kiwango cha elimu kilichopevuka na uadilifu.

“Baraza hili linamiliki mali zinazohamishika na zisizohamishika na sisi ndiyo tunachukua uhimizwaji wa kuulizwa na kudodoswa kila kilichopo ndani ya Bakwata kwa kuwa ni lazima tuhusishwe hususan katika masuala ya elimu,” alisema Habibu.

Kwa mujibu wa maelezo ya Katiba, vikao hufanyika mara mbili kwa mwaka chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Maulamaa pamoja na vikao vya dharura. “ Januari 3, 2011, tulifanya kikao cha kawaida ambacho kilikuwa na agenda tatu ikiwemo ya umuhimu wa kujenga chuo Kikuu cha Kiislamu ambapo wajumbe walipendekeza kijengwe katika maeneo ya Dodoma, Tanga ama Chang’ombe.”

“Kutokana na mapendekezo hayo, tuliafikiana kijengwe Chang’ombe lakini ikaonekana kuwa Chuo Kikuu cha Kiislamu kinahitaji sehemu kubwa na pale kuna Ekari 4 hapatoshi,” alisema shahidi huyo wa pili wa upande wa mashtaka.

Hivyo walimtaka Katibu Mkuu wa Baraza la Maulamaa na timu yake wafanye mchakato wa kutafuta eneo maalumu kubwa ambalo wataweza kujenga chuo hicho Kikuu cha Kiislamu na kwamba baada ya siku nne au tano walipigiwa simu na kuwa wanahitajiwa Makao Makuu (Bakwata).

Shahidi huyo alidai kuwa walipofika waliambiwa kuwa kuna kikao cha dharura na kupatiwa taarifa na Katibu Mkuu wao juu ya mchakato huo wa kutafuta eneo kuwa kampuni ya Agritanza Ltd ilijitokeza na kutaka tuwape zile ekari nne na wao watupe ekari 40 huko Kisarawe Pwani.

“Sisi tuliona ekari 40 kwa ekari 4 ni kama ardhi na mbingu na Mungu alisikia kilio chetu akawaleta hao na tukaona kabla ya mazungumzo twende tukaone, tulipofika Manshalaa eneo lilikuwa sehemu nzuri, linapendeza, linavutia na mimi nilikuwa wa kwanza kuwashawishi wenzangu tukubaliane na mabadilishano na mchakato ukafanyika,” aliongeza shahidi huyo mahakamani hapo.

Hivyo Baraza la Maulamaa liliridhia kutoa maamuzi kwa Baraza la Wadhamini kufanyika kwa mchakato na makubaliano wa maeneo hayo.